Monday, February 28, 2011

MTOTO WA BANANA ZORRO.. LIKE FATHER LIKE SON!!!

Huyu ni SON wa Banana Zahir Ally Zorro, mara ya kwanza nilivyomuona pale uwanjani nilihisi ni katoto ka kike kumbe NI WA KIUME.. nafkiri hata wewe ukimuangalia tu utakubaliana na mimi.. kamekaa kama kasichana kabisa yani.. SO CUTE!!! naona mzee zorro ana product za ukweli...
Hapa akiwa na Baba yake, LIKE FATHER LIKE SON.. wakati nafanya kipindi pale uwanjani nikiwa naruka live on Clouds FM, aliniona nimeshika MICROPHONE sasa sijui alijua ni ya baba yake maana alinifuata na kuanza kuninyang'anya huku akilia akiwa anaitaka yeye ile MICROPHONE ikabidi nimuachie tu kwa muda lakini kumnyang'anya ilikuwa kazi kubwa baadae..
Hapo ndio ninaposema like father like son coz alichanganyikiwa kabisa baada ya kuiona MIC na ukizingatia kazi ya baba yake inahusisha Microphone so huenda kuna vielement flani vya baba ama familia historia inajieleza.. TUNASUBIRIA lol!!
Hapa akiwa na baba yake.. SAAAAAFIIIIIII!!!!!

MATUKIO KATIKA PICHA.. MECHI YA BONGOFLEVA NA WANAFILAMU!!!

Hii ilikuwa ni nyomi la siku ya mechi ambayo ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kuchangia wahanga wa mabomu ya gongolamboto

Hii ilikuwa ni kamati ya Ufundi kwa upande wa filamu ambao kiukweli kabisa sikuelewa kazi yao ilikuwa nini maana walitundikwa MBILI BILA tena katika style ya Tembo na Sisimizi

Hakuna watu walikuwa na mbwembwe kama watu wa filamu.. kabla ya wachezaji kuingia walitangulizwa hao unaowaona na matunguli yao uwanjani ambapo hiyo ndio kamati ya ufundi iliyoweka kambi yake BAGAMOYO lakini matunda yake hayakuonekana.. kutoka kushoto ni BI MWENDA, MBOTO, DOKII, CHOPA, MZEE CHILO na MZEE MAGALI.

hiki ndio kikosi cha timu ya Bongofleva ambao kwa kuwaangalia tu kiukweli wanaonekana proffessional na wamejipanga, kikubwa hawakuwa na mbwembwe kabisa lakini waliwanyamazisha vibaya watu wa filamu... mh! ila walipania..


WANAFILAMU ndio hao kama unavyowaona na kikosi chao.. Weeeeengiiiiii wenyewe lakini zilikuwa ni mbwembwe za bure tu, mwisho wa siku walirudi vichwa chini.. THOUGH naomba niseme kwamba AKUNA TIMU ILIYOCHANGAMSHA UWANJANI KAMA WATU WA FILAMU.. wao ndio walikuwa na matukio mengi sana ya kufurahisha wakati wanamuziki walikuwa kikazi zaidi..wao ni mpira na wao wao na mpira na walionesha kiwango kwelikweli..

WEMA SEPETU pamoja na JACKY PENTZEL nao walikuwepo ndani ya uwanja
Hapo sura zetu ndogoooo, la kuongea tena hatuna tumeshalishwa magoli yetu tumetulia yaliyokuwa yakiendelea hapo ni maneno ya mkosaji tena katika mazungumzo baada ya habari.. mh! tuliwezwa maana mwenyewe nilikuwa upande wa filamu, kutoka kushoto SAJENT, AUNT EZEKIEL, ZAMARADI MKETEMA, FLORA MVUNGI huyo aliyejishika kichwa pamoja na MONALISA hapo chini...

MSOSI POPOTE ...
DEOGRATIUS SHIJA nae alikuwepo.. kilichonifurahisha ni jinsi WATANZANIA walivyoitikia wito.. kiukweli kabisa ilikuwa ni kitu kizuri sana.. BIG UP kwa watanzania wote, Big up kwa WACHEZAJI WA TIMU ZOTE na pia kwa CLOUDS MEDIA GROUP kwa kuratibu kitu kikubwa kama hiko ambacho matunda yake yameonekana...
kutoka kushoto SAUDA MWILIMA, SAJENT, AUNT EZEKIEL na mimi huko kulia mwenye kofia..
Washabiki..
DIAMOND pamoja na DOGO JANJA wakifurahia ushindi wao...
Timu ya BONGOFLEVA ikiongozwa na H-BABA wakifurahia Goli... walitunyoosha kisawasawa tuliokuwa tunashangilia filamu..
Watu wa filamu tulikabwa sana siku hiyo...hapo mtitu (mwenye nyekundu)akijaribu kufurukuta mbele ya mwana ubongo wa fuleva...
Mstahiki meya wa Ilala JERRY SLAA kushoto pamoja na Mheshimiwa mbunge wa Kinondoni IDDI AZZAN pamoja na RUGE MUTAHABA ambae ndio alikuwa mratibu wa shughuli nzima..


BANANA alikuja na MTOTO WAKE uwanjani.. mwanzoni nilijua huyu mtoto ni wa kike.. and i was so suprised aliponiambia ni MTOTO WA KIUME maana ilibidi nimuangalie mara mbilimbili.. ni kacute sana.. naona product za mzee Zorro sio mchezo
MOHAMMED MWINKONGI (Frank) nae alitia maguu akiwa na mali yake..
hakuna mtu alienichekesha kama MASANJA ambae yeye alichezea timu ya filamu lakini baada ya kufungwa akajifanya kwamba ni MUIMBAJI na sio muigizaji hivyo akajaribu kubadilisha jezi lakini wakamvua na kumrudisha kwenye jezi yake nyekundu..
Kiushabiki zaidi.. NATASHA na mwanae MONALISA, na kule mwanzo mwenye T-shirt ndefu COLETHA..



Hii ilikuwa ni siku nzuri sana aisee, uwanjani kulikuwa na vituko vingi sana especially style ya uingiaji ya wachezaji wa filamu ambapo MASANJA alikuwa akitembea ule mwendo wake wa kizembe wakati JOTI alikuwa akisalimia mashabiki huku akishhtu.. BIG UP kwa WASANII WOTE kwa moyo wao wa kujitolea kwa ajili ya ndugu zetu hawa wa Gongolamboto bila kusahau WATANZANIA waliojitokeza kwa hali na mali pamoja na CLOUDS MEDIA GROUP.. wanastahili pongezi!!!

Friday, February 25, 2011

ITS NOT ONLY ABOUT BEAUTY.. ITS BRAIN & BEAUTY or BEAUTY WITH PURPOSE" - Sporah Njau

SPORAH NJAU, is an award-winning the best TV Presenter of the year 2010.

In the city of London here comes a young vibrant lady full of life and enthusiasm always ready to go above her abilities to deliver the best. Miss Sporah Njau believes you can do it. Her positive spirit led her to an unending array helping young people in the community to speak out in different issues.

Miss Njau is a hardworking lady who believes in education more than anything else, with a heart of her career as a TV presenter/producer. Miss Njau came from a humble background to become one of the African most influential lady in United Kingdom. She has amassed a great fortune through her media interests and uses her TV Show to positively influence of the young generation.
Sporah Njau, who has a background in business and higher education, has lived in United Kingdom for seven years. She has a High National Diploma in TV Presenting, BTEC in Business and Finance and HND in Accounting and Business Management.
Business was her foundation; her 1st business while studying was 2005, When she started her online retail, selling Wigs, hair extension and African Sandals.

As she heads up the accelerated degree programs, Sporah found her passion in TV Presenting.

In 2010 Sporah achieved her Bachelor Degree in International Business Management from London Metropolitan University.

After watching different TV talk shows, Sporah realised how powerful TV is, and how it can influence or change people's life especially the young generation. So she came with an Idea of a TV Talk Show.

In August 2007, The Sporah TV Show was born, the show discusses issues that affect the Black African community residing in UK and Europe and Africa as a whole.

Currently, The Sporah Show is a weekly talk show shown in Europe and Africa (East-Africa). In Europe SKY Channel 184 BEN Television, every Monday at 9:30pm and in Africa (Tanzania) every Friday at 18:00pm and Saturday’s at 13:00pm on STAR TV in Tanzania.
In 2009, The Sporah Show was nominated for the Best TV Show and The Best TV Presenter of the year on BEFFTA Awards. And in April 2010 The Sporah Show received Awards for the contribution to the African Community in the UK.

In September 2010 The Sporah Show was nominated for the Best TV Show, Best TV Personality and The Best TV Presenter on BEFFTA Awards. December 2010 Sporah won award for the best TV Presenter of the year 2010
Sporah is passionate about the things that interesting her. Her job, family, her local church and community.

THE GOOD MOMENT OF HER ilikuwa siku ya kwanza kuiona Sporah Show kwenye TV, anasema alitoa machozi ya furaha! kwani ilikua ngumu sana kwake kuamini ukizingatia kulikua na vipingamizi vingi sana. Na pia siku aliyo graduate, hakuamini kama angeweza na hio ni kutokana na challenges alizokuwa anapata wakati yuko university kwani haikuwa kazi rahisi kwake kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja ambapo alikua AKISOMA huku akiendelea KUPRODUCE KIPINDI.
THE BAD MOMENT always ni pale anapokua amealikwa mahali ambapo hapahusiani na kazi zake hasa na marafiki zake wa karibu halafu akashindwa kwenda kwasababu ya kazi zake zisizoisha, huwa anajiskia vibaya sana kuwaconvince marafiki zake wa karibu hakuweza kuwa nao most of the time

KITU AMBACHO HUFAHAMU KUTOKA KWA SPORAH
Kwanza kabisa, She believes in GOD, she is a loving person, very easy to get along with.. very Simple, so caring, hard working and a risk taker.
Kitu kimoja ambacho angependa watu wajue ni kwamba amekutana na changamoto nyingi sana kwenye maisha yake na anaendelea kukutana nazo ila anajitahidi kukabiliana nazo kadri ya uwezo wake.

Nilimuuliza katika hizo challenges ambazo ameshakutana nazo anaweza akakumbuka nini kilichowahi kumkwaza na hivi ndivyo alivyonijibu...
"The few once that i can remember is: I was Young Black African woman from Tanzania!! Trying to do a TV Show!!! It was very very very hard to convince people here in London, even close people around me. Secondly, I had problem with a Language barrier.. Ila sikuona kama huwa Afrian au kutokuongea English ni Kilema/Disability!! Niliyaweka yoote pembeni na ku focus na kile nilichokua nataka kuachieve. Ninachojaribu kusema ni kwamba USIKUBALI MTU AKUAMBIE KWAMBA HUWEZI KUFANYA KITU AU HUWEZI KUFANIKIWA NO.. Ukifanya kazi utavuna unachopanda na Mungu hamuachi mja wake."
UJUMBE WAKE KWA WADADA...
"And for my Ladies! I so much believe that the world we are leaving nowadays its not only about beauty! not anymore. Now Its "Brain & Beauty Or Beauty with Purpose" and not just beautiful."

Cha mwisho kabisa SPORAH anapenda ssaana kupika kuliko kawaida, so mda wowote anaopata nafasi huutumia kufanya hivyo...

Kipindi cha sporah huoneshwa kila ijumaa saa 12 jioni na kila jumamosi saa saba mchana kupitia Star TV na pia Unaweza ukamtembelea kupitia blog yake ambayo ni http://www.thesporahshow.blogspot.com/ ns pia http://www.sporahshow.com/ pia kupitia facebook, twitter na youtube unaweza kujionea baadhi ya vipindi vyake ambavyo huwa anafanya...

Thursday, February 24, 2011

NIMEONA NIZITUPIE TU PICHA ZANGU MAANA NAONA HAZINA MATUMIZI.. IJUMAA NJEMA JAMANI!!!!

Ukuniuliza nini napenda, nitakujibu picha.. naomba nikiri hilo!!! Hivi vipicha vilikuwepo tu nikaona si vibaya nikavitundika humu ukizingatia sina matumizi navyo yoyote!!!
Zamaradi mpenda picha
Ukiangalia unaweza ukaona kama zinafananafanana hivi lakini nilichoona niziweke tu zote...
Wanasema kununanuna hovyo sio kuzuri kwa afya.. sura inazeeka, so always smile, matatizo yapo kila siku usiyaendekeze!!!

mpenda picha...
Hii ilikuwa kama miezi minne hivi iliyopita...
IJUMAA NJEMA JAMANI.. NAWAPENDA WOOOOTE, MNAONIPENDA NA KUNICHUKIA.. TUKO PAMOJA!!!!

MICHAEL JACKSON ALIVYOFARIKI NILILIA SANA - MC KENYATTA

Anaitwa MC kenyatta ambae ni muigizaji wa filamu wa hapa Tanzania lakini at the same time ni Dancer mashuhuri wa enzi hizo ambae alikuwa akipenda sana kucheza nyimbo za King of pop Michael Jackson....
Kenyatta anasema wakati MICHAEL JACKSON anaumwa alikuwa na unyonge wa hali ya juu na aliposikia habari za kifo chake ALILIA KULIKO KAWAIDA...
Na sababu kubwa iliyomfanya alie sana ni mapenzi yake ya dhati kwa MJ (Michael Jackson).
Baadhi ya CHEJO zake za Ki-MJ... hapo alikuwa ananitolea show ya ukweli ya Michael Jackson
Ukimuuliza SABABU KUBWA iliyomfanya ampende MICHAEL JACKSON, Mc Kenyatta anasema sababu kubwa ni kwakuwa MICHAEL JACKSON ALIKUWA AKIPENDA SANA WATOTO na kwa matatizo aliyoyapata yeye utotoni anatamani sana MICHAEL JACKSON ANGEMUONA AKAMCHUKUA ili aondokane na shida hizo, hivyo alikuwa akimuangalia MICHAEL kama mkombozi fulani.. na kingine alikuwa akipenda anavyocheza...

UNAWEZA UKASHANGAA SHIDA GANI ALIZOPITIA LAKINI KUNA SIRI KUBWA SANA NYUMA YA MAISHA YA MC KENYATTA AMBAPO NTAKULETETEA HALI HALISI YA MAISHA YAKE MUDA SI MREFU ila kwa DONDOO tu ni kwamba hivi unafahamu alivyokuwa mdogo ALIIBWA KUTOKA KWA MAMA YAKE MZAZI NA AMEKUWA AKILELEWA NA MAMA AMBAE SIO WAKE KWA MUDA WOTE HUO ( ALIEMUIBA) na hivi sasa ANAMTAFUTA MAMA YAKE MZAZI!!!.. kwa yote haya endelea kuwa na mimi ndani ya blog hii na nitakuletea kisa cha maisha yake kama kilivyo....

Lakini pamoja na yote hayo MC KENYATTA pia ni MC mashuhuri sana wa sherehe mbalimbali kama MAHARUSI, SEND-OFF, VIPAIMARA na shughuli yoyote ile na huwa anaimudu sana kazi yake kama MC kwani ni mtu ambae hufurahisha sana anapofanya shughuli hizo na mara nyingine hutoa hadi hizo SHOW za Michael Jackson katika kuchombeza.. hivyo kama una harusi yako, send-off, Ubatizo, Birthday, Kipaimara ama SHEREHE YOYOTE ILE unaweza ukamcheki kupitia namba zake za simu ambazo ni 0715-226005 au 0754-226005 ama 0689-226005. na anaweza akafanya sherehe yako iende sawa kabisa..

JACKUELINE NTUYABALIWE IS THE MOST BEAUTIFUL WOMAN IN THE WORLD - TK... UZURI WAKE WALETA GUMZO

Kupitia mtandao wa facebook TEDDY KALONGA (TK) ametoa compliments kwa JACKUELINE NTUYABALIWE na amekiri kwamba kwake yeye mpaka sasahivi anafikiri JACKUELINE NTUYABALIWE ndio mwanamke mzuri kuliko wote duniani, na hiyo aliiandika kama kitu kilichokuwa kwenye fikra zake kwa muda ule na status yake ilisomeka kama hivi.. "I still think Jacqueline Ntuyabaliwe (K-LYINN) is the most beautiful woman in the world. ♥ ♥ ♥ I miss her. " kitu ambacho kimeibua ka-gumzo kwa watu kwa kila mtu kucomments anachokiona kuhusiana na hilo...
Baada ya kuandika hivyo TK alipokea comments nyingi sana kutoka kwa watu mbalimbali wengine wakisupport, wengine wakiwa tofauti kidogo na wengine wakitaja watu ambao wao kwa mtazamo wao wanafikiri ni wazuri zaidi ya K-lyn ambapo katika hao hata TK mwenyewe alitajwa
Hapo akiwa na Hoyce Temu

Ukiachana na TK mwenyewe kuna mtu alikubaliana naTK kwamba K-Lyn ni mwanamke mzuri lakini si kwa dunia nzima ila alichokisema ni kwamba kwa upande wake HOYCE TEMU ndio namba moja halafu anafatia K-lyn ambapo comment yake ilisomeka kama ifuatavyo.. "in the world...no! But she is beautiful...to me wa pili kwa uzuri kwa miss tz walioshika taji,hoyce temu then jacquline"


wakati comments zikiendelea kuna mtu ambae alisema ye kwake anamuona kawaida tu sana na alichoandika ni kama hivi "mmmmhhhhhh sijaona kawaida tu teddy or rangi na uchotara,......but u r cute than her tedy sorry to say tha" kitu ambacho TK alikipinga kidogo na kuelezea kuwa yeye K-lyn kwake bado ni msichana mzuri hata angekuwa vipi kwa kusema "me I think hata angekuwa mweusi kakekuwa bado kazuri tu. Have you seen her lips, eyes, her teeth, the way she talks omg. :))" na akapata support kwa mtu ambae alisema JACKUELINE NTUYABALIWE ataendelea kuwa miss wake of all time!!!
Kwa upande wangu mimi naomba niwe mkweli tangu nikiwa mdogo nimekuwa nikimuangalia K-LYN kama mtu (msichana) anaenivutia sana, sura yake, umbo lake, anavyovaa na the way alivyo kwa ujumla...

Kikubwa kingine kinachonifanya niendelee kumkubali zaidi na zaidi ni kwakuwa KILA ANAVYOZIDI KUKUA NDIVYO UZURI WAKE UNAVYOONGEZEKA... mara nyingi watu hasa wasichana umri unavyosogea na uzuri unakua kama unapungua hivi lakini kwa JACKUELINE NTUYABALIWE imekuwa kama tofauti kwani yeye kadri umri unavyoongezeka na uzuri wake unazidi kiufupi anajua kuji-maintain which is good.. so kwangu mimi K-LYN ni mmoja kati ya wanawake wazuri sana... SHE IS BEAUTIFUL kwakweli...
Baadhi ya picha zake akiwa katika pozi tofauti.. look at her smile na structure ya sura yake!!!
Hapa akiwa amekata nywele...
FULL SIZE PICTURE
In different pozi.....

Hii ni moja kati ya Show alizowahi kufanya kama mwanamuziki enzi hizo.. i dont know why simsikii kwenye music siku hizi... kila mtu ana strength zake, unaweza ukawa si mkali sana kwenye kitu fulani lakini ukawa na kitu ambacho mwingine hana na hiko kikafufanya u-stand out na kukubalika..

Moja kati ya vitu vilivyokuwa vikimbeba k-lyn kwenye music ni uzuri na mvuto wake, utatamani kuangalia videos umuone alivyovaa na alivyo.. PERSONALITY is everything katika kazi ya sanaa, na alikuwa nayo kitu kilichomuongezea credits zaidi.

Another beautiful chick and fashionista as well TEDDY KALONGA (TK) ambae ndie amemuona NTUYABALIWE kama mwanamke mzuri duniani..
Huyo ni TK.. na wanasema uzuri wa mtu uko machoni mwa mtu na TK ameona kama K-lyn ni the most beautiful woman in the world...
KWA UPANDE WAKO NI MWANAMKE/MSICHANA GANI ANAEKUVUTIA SANA HAPA BONGO NA NINI AMBACHO KINAKUVUTIA ZAIDI KWAKE!!!!!!?????