Thursday, July 28, 2011

NYUMA YA CAMERA YA TAKE ONE!!!

Kipindi cha TAKE ONE mpaka kikamilike huwa kuna watu wengi ambao wanafanikisha hilo, kazi yangu mimi huwa ni kutafuta materials, kujua nini cha kufanya kwenye kipindi kama producer pamoja na kukipresent nilichokiandaa..

Swala la mwanga sijui umekaaje, upigaji picha pamoja na Set huwa sishughuliki nayo ila kuna watu ambao wao ndio wanafanikisha hilo, watu ambao tunafanya kazi kwa upendo na ushirikiano mzuri kabisa pamoja na masikilizano... watu ambao huwa nyuma ya camera kila wakati ambao tunarekodi na wana mchango mkubwa sana pia kwenye kipindi sababu siwezi kujipiga picha mwenyewe..

Nawazungumzia macameraman wawili ambao wanaijua kazi yao vizuri sana REGINALD MARO (p.diddy) pamoja na RAYMOND CHARLES..

Mbali na kuwa wafanyakazi wenzangu kwangu mimi hawa watu wawili ni kama Brothers kabisa kutokana na jinsi tunavyoishi kwa upendo na bila unafki wowote.

kupitia blog hii leo nimeamua kushow love kwao sababu wanastahili..

SALUTE!!

Tuesday, July 26, 2011

I LOVE THE HAIR mama Jonii.. Looking soooooo GOOD!!

Kiukweli nimezipenda hizi nywele sana, zimekupendeza mnoo. .. I love them for real!!!
nimeipenda hii picha jinsi ilivyo ilivyo tu... mama jonii unatisha!!!

Saafi.. looking Gorgeous kwakweli!!!

COMING SOON!!!

FOR SALE......!!!

Kuna mdau kanitumia hii kupitia facebook, kwa yeyote anaehitaji awasiliane nae kupitia 0714766077
Haya jamani kazi kwenu!!

Friday, July 22, 2011

IJUMAA KARIM...

kwa wale wapenzi woote wa blog hii, nawatakia Ijumaa njema..

NAWAPENDA WOTE

THANKS FOR THE COMPLIMENTS MISSIE POPULAR..

Katika pitapita zangu leo kwenye blogs tofautitofauti ghafla nikakutana na hii post ambayo iliwekwa na missie popular.blogspot.com siku ya july 15, 2011 ambayo ni ijumaa iliyopita lakini mimi nimefanikiwa kuiona leo sikuwahi kuiona kabla, hivyo sina budi kumshukuru kwa kuona alichokiona kwangu.. na alichokiandika kuhusu mimi ni hiko hapo chini

"Random- Zamaradi Mketema
A diva from Clouds TV and one of the best dressed popular people that i know,from Tanzania! She has an amazing voice and such a talent and deep understanding of the movie industry in the country!Today, lets check her trends;
"

Na baada ya hapo akaweka picha zangu tofautitofauti na katika picha alizoziweka mojawapo ni hiyo hapo chini..






Na akamalizia kwa kusema
"In short,she is a trend setter,and we love that about her....Popularized!!!"


Sio maneno yangu ni ya mtu mwingine kabisa kuhusu mimi na Kiustaarabu mtu anapokucompliment kwa chochote hata kama ni kidogo kiasi gani ni lazima uoneshe kuthamini..
hivyo sina budi kusema Thanks for the compliments..


I APPRECIATE!!


Thursday, July 21, 2011

THT WAKIWA KWENYE REHEARSALS ZINAZOENDELEA HUKO AMERICA..


NAMISS MUZIKI WA HUYU MTU, NATAMANI KUMUONA TENA KWENYE GAME...


Ukizungumzia mashabiki wa ukweli mpaka sasa naweza nikasema mimi ni mmoja kati ya mashabiki wakubwa sana wa Mr. Nice mpaka sasa.

Inaweza ikawa kama hujanisoma kutokana na mashabiki wake wengi kuwa watoto lakini kiukweli kabisa huyu ni mmoja kati ya wanamuziki ambae aliweza kuteka kundi kubwa sana la watu kupitia muziki wake na kupitia watoto pia ambapo asilima kubwa ya wazazi walijikuta wakimpenda Mr. nice kupitia watoto wao.

Naomba nikiri kwamba mpaka sasa nnaposikiliza mziki wake naendelea kupata hisia ileile ambayo nilikuwa nikiipata enzi hizo ambapo nyimbo zake ndio zilikuwa HIT songs.
Mr. nice alikubalika sana hadi nchi jirani na alikuwa na heshima kubwa mno kwenye nchi hizo ambapo mbali na uimbaji wake vilevile alikuwa akijituma kwenye Stage..

Pamoja na kwamba anaendelea na muziki na kwasasa anafanya live band lakini Naomba nikiri kwamba namiss muziki wa huyu mtu na natamani sana arudi tena kwenye game siku moja kama ilivyokuwa enzi hizo zamani kwani yeye ndio mwanzilishi na mtu wa kwanza kabisa kutambulisha style ya TAKEU na alivuma sana na nyimbo zake kama FAGILIA, KIDALI PO,FRIDAY NIGHT, MAMA, KING'ASTI, FIRST LADY, KIKULACHO ambayo ilikuwa maarufu sana Uganda, BWANA SHAMBA, RAFIKI ambao ni huo wa kwanza hapo juu na moja kati ya nyimbo ninazozipenda kutoka kwake na nyinginezo nyingi sana.

Nyimbo zote hizo zilimpa mafanikio na umaarufu mkubwa sana kwa watoto mpaka watu wazima na kingine kikubwa ilikuwa ni style ya Uchezaji aliyoitambulisha yeye ambapo watoto ulikuwa huwaambii kitu, mtoto akicheza tu basi style ni hiyo bila kujali wimbo ni wa mr. nice ama la.

Fanya kama unawaza tu mtu kama huyu ambae alikuwa ni kipenzi cha watu wengi na hajaonekana kwenye majukwaa makubwa kwa muda mrefu halafu ghafla tu unamuona sehemu kama FIESTA akiperfom HIT zake za enzi hizo, unahisi ataamsha hisia za watu wangapi!!???

WATOTO BWANA.. HEBU ICHEKI HII.. !!!

HONGERA DA SUZY (MARYAM)....

Tulimzoea kwa jina la Susan Baltazary (da Suzzy), lakini kwasasa anajulikana kama Maryam Baltazary ambae mwishoni mwa wiki alifunga ndoa na Eddy Ramadhan katika jiji la TANGA...
Hongera sana...

Tuesday, July 19, 2011

AISHA MADINDA AIKIMBIA TWANGA PEPETA NA KUHAMIA EXTRA BONGO..

Katika kile ambacho hakikutegemewa na wengi, mnenguaji wa siku nyingi sana ambae alikuwa akiifanyia kazi Twanga Pepeta Aisha Mbegu maarufu kama Aisha madinda ameihama rasmi Bendi hiyo ya The African Stars Twanga Pepeta na kukimbilia Extra Bongo ambayo iko chini ya Mzee wa Farasi ally choki..
Akitambulishwa rasmi kama mwana Extra Bongo..
sababu kubwa aliyoitoa Aisha alisema ni kutokana na safu ya wacheza show wa Extra Bongo ambao wengi wao amewazoea na amefanya nao kazi siku nyingi sana hivyo kukutana nao tena huku kutamfanya awe comfortable zaidi na kazi yake..




Kabla ya Aisha kuhamia Extra Bongo akitokea Twanga, tayari Extra Bongo ilikuwa imekwishanyakua wanenguaji wengi kwa mpigo kutoka Twanga akiwemo kinara nyamwela, Super danger, otilia pamoja na wengineo hivyo huenda hao ndio aliomaanisha aisha madinda kwamba ndio watu aliowazoea!!

THT in America...


Kwasasa wasanii kutoka Tanzania House of talents THT Mwasiti, Linah, Barnaba na Amini wako Marekani ambapo wanatarajia kuimba jukwaa moja na Usher raymond ambayo itakuwa ni kwaya ya watu 14.


Hizo ni sehemu za rehearsel wanazoendelea kufanya wakiwa huko
Na hiyo itakuwa ni historia nzuri sana kwenye career yao ya muziki kuimba jukwaa moja na Usher raymond ambae ni msanii mkubwa sana Duniani..
All the best guys!!!

Sunday, July 17, 2011

WIMBO WA LEO - MSIACHE KUONGEA

TAMKO LANGU..

JICHO LA TATU - TUTAFIKA KWELI?
Nimeona nirudie tu kitu ambacho niliwahi kukiandika nyuma lakini kwa kuongezea baadhi ya mambo pia
Katika Entertainment Industry hapa Tanzania kuna fani tofautitofauti, lakini zile ambazo zinaonekana ziko juu zaidi na zinachukua attention ya watu wengi ni MUZIKI, MITINDO na FILAMU.

Nikianza kuzungumzia Industry ya Filamu ni kitu ambacho kimekua juu ghafla tu miaka ya hivi karibuni, tofauti na Muziki ambayo ni Tasnia kongwe zaidi, Na Industry ya Filamu imeshatoa watu wengi sana ambao mpaka sasa ni MA-STAR WAKUBWA MNO hapa Tanzania na wanaendelea kufanya vizuri.

Kuna Usemi Usemao HATA MBUYU ULIANZA KAMA MCHICHA ambapo maranyingi huwa tunatumia msemo huu kujifariji na kujipa moyo pale ambapo tunaona mambo yanaenda ‘Slow’ ama tofauti na matarajio yetu. Lakini tukumbuke vilevile kwamba NYOTA NJEMA HUONEKANA ASUBUHI na DALILI YA MVUA NI MAWINGU, kwa upande wa wasanii wa Filamu wanaonesha hakuna kabisa dalili ya mabadiliko kati yao, wanaridhika haraka na kusahau walipotoka. Ili kuweza kufanikiwa katika vitu tunavyovifanya siku zote ni Vizuri kuangalia ‘NEGATIVES’ zetu zaidi kuliko ‘POSITIVES’ sababu kwa kuangalia mabaya na udhaifu wetu itatusaidia kuendelea mbele zaidi kwa kurekebisha tunapokosea kuliko mazuri yanayotufanya tubweteke na kuamini kwamba kilakitu kiko sawa wakati huenda ikawa tofauti.

Ili fani zote hizo ziweze kuendelea mbele kuna kitu kimoja kikubwa kinachohitajika sikuzote ambacho ni MEDIA kwa maana ya Vyombo vya habari kama Television, Radio, Magazeti, Mitandao n.k. Kupitia Vyombo vya habari watu ndio wanatambua uwepo wa watu ama kazi Fulani.
Business without advertising ni kama kumkonyeza mtu gizani. Hata kitu chako kiwe kizuri namna gani lakini kama watu hawakifahamu hakitakuwa na faida yoyote, It’s useless. Hivyo kazi kubwa ya Media ni kuripoti habari na mambo mbalimbali yahusuyo tasnia tofautitofauti ikiwemo na WAHUSIKA WENYEWE.

Ikumbukwe kwamba si kuripotiwa kwa MAZURI TU MNAYOYAFANYA bali hata pale MNAPOKOSEA media haitakuwa nyuma kwa hilo. Na hio ni kwasababu tu unapokuwa mtu maarufu wewe ni kioo cha jamii na kama kioo cha jamii watu watataka kujua mengi sana kuhusu wewe sababu kuna wanaotamani pia siku moja wawe kama wewe. Hivyo kama umeamua kuwa Star SAHAU kuhusu PRIVACY.

Lakini kwa upande wa BAADHI ya wasanii wa filamu ambao wao ndio wangeweza kuwa muongozo kwa wenzao hali inasikitisha kidogo, Inaonekana kabisa kwamba wanasahau WALIPOTOKA, Wanasahau kwamba VYOMBO VYA HABARI ndio vimewafikisha hapo walipo, wanasahau pia kwamba wao ni vioo vya jamii hivyo kila wanalolifanya jamii inataka kujua nini kinaendelea katika maisha yao.

Ombi langu tu kwa YEYOTE anaehusika msiifanye hii fani ikaonekana kama ni ya watu waliokosa muelekeo wa maisha wakaona njia pekee ni kukimbilia huku hapana. Baadhi yenu Reaction zenu zinaonesha udogo wa IQ zenu na hiyo inatukanisha moja kwa moja tasnia yetu hii nzima ya Filamu tukichukua kauli ya Samaki mmoja akioza ni wote wakati kuna wengi ambao wanajua nini wanakifanya. Kwenye hiyo ni kama inawaharibia. Filamu ni Ulimbukeni na Ujuaji mtupu uliojaa huku.

Hebu jiulizeni kuna Mastar wangapi wakubwa hapa Tanzania wame-struggle mpaka kufikia walipofika si kijina tu bali hata Kiuwezo na bado wanaheshima na kuheshimika katika jamii, hawajisahau. Mfano mzuri ni lady Jaydee ambae ni mwanamuziki, This is a real Diva na mfano mzuri wa kuigwa na watu wa tasnia zote kwa sasa, mafanikio yake yanaonekana waziwazi na hiyo ni kutokana na msingi mzuri aliojiwekea , lakini mbona hana majigambo na hizo Showing off za kienyeji!!! I RESPECT THIS WOMAN. Sidhani kama angekuwa na hizo mbwembwe mlizonazo angefika hapo alipo.
Mnachotakiwa kujua ni NO ONE IS PERFECT, kila mtu hukosea si wewe wala mimi, hata wakubwa wa nchi hukosea pia maranyingine na ndiomana kukawekwa washauri, Ubinadamu ulizingatiwa.

Sasa wewe unapokosolewa DON’T TAKE IT PERSONAL sababu hakuna mwenye Chuki na wewe, lengo ni kujenga na si kubomoa, WEWE NI NANI mpaka upambwe kila siku!? Mbona mnapenda SIFA tena zile za kijinga?? Badilikeni jamani ni aibu, nafikiri mngekuwa mnajua mastar wenzenu wa ulaya wanaishi vipi sidhani kama mngelalamika eti kwa KUKOSOLEWA FILAMU.

AMKENI JAMANI, nafikiri wengi wenu HAMJITAMBUI!!, hamjijui nyinyi ni wakubwa kiasi gani, mngelifahamu hilo msingekuwa na hoja za kitoto kama ambazo wengi wenu mnazo, nyinyi ni VIOO VYA JAMII, mtu yoyote ambae ni kioo cha jamii hawezi kufanya madudu hadharani na watu wakakosa kuongelea (media) sababu hauko kwa ajili ya familia yako, ila uko kwa ajili ya jamii nzima, na unapoongelewa HUKO SIO KUINGILIA UHURU WAKO na wala hakuna mwenye chuki na wewe, mtu akuchukie kwa kipi!!??? ama Mnakutana wapi!!?? anakuongelea kwasababu wewe unastahili kuwa mfano kwa wengine wengi ambao wanakuangalia,wewe ni Public figure..

Kumbukeni kwamba hapahapa TANZANIA tu kuna aina fulani ya watu(a certain class of people) ambao bado hatujafanikiwa kuwateka kuangalia hizi filamu zetu, mkatae mkubali hili liko wazi, na kazi kubwa inayotakiwa kufanywa ni kuangalia jinsi gani tutawavuta hawa ili wote tuwe kwenye boti moja, HATULAUMIANI kwenye hili kwani industry yetu bado changa sana, lakini pamoja na uchanga wa industry yetu, tusioneshe basi kwamba hata akili zetu ni changa pia katika kuchanganua mambo jamani, nyinyi ni wakubwa MNO na mnaangaliwa na watu wengi sana hivyo acheni utotoutoto na KUJI-HISIHISI kusikokuwa na sababu.

Mara nyingi huwa tunajipa moyo tunavyoona filamu zetu zinakubaliwa sana nchi jirani kama RWANDA, BURUNDI na CONGO.. labda niwape siri moja kwamba sababu kubwa ya kufurahiwa hivyo ambavyo tunafurahiwa ni kwasababu ya LUGHA YA KISWAHILI ambayo tunaitumia na wao wanaielewa kirahisi na si kwamba filamu zetu ni nzuri saana kupita wengine, na ndiomana nchi kama UGANDA ambao ndio tuko karibu nao zaidi Hatupokelewi kihivyo kama ilivyo nchi hizo nyingine(language barring)...
Pamoja na kwamba hiko ni kitu cha kujivunia (kupokelewa kwetu vizuri) tusibweteke basi badala yake tuongeze juhudi ambazo hata mtu ambae haelewi lugha yetu akae chini na kuangalia na kusema hii ninayoangalia ni filamu, sababu itafika muda watazoea wataona kawaida na watachoka kwani hata kama kitu ni kizuri kiasi gani lakini kama ni kilekile kilasiku KINACHOSHA na ndiomana hata sisi tumezichoka za NIGERIA kwasasa lakini miaka kadhaa nyuma ilikuwa huambiwi kitu kwa filamu hizo za Kinigeria.. Tujaribu kuwa flexible na tukubali mabadiliko.

Lack of exposure ndio tatizo kubwa linalowakibili wengi wenu, Exposure ni kitu kizuri sana jamani, tusiishie NIGERIA tu, hebu tujaribu kuangalia mbali zaidi, siku zote siri ya mafanikio ni kuangalia wenzenu walioendelea kwenye kitu Fulani wanafanya nini juu ya jambo husika, Hakuna ubaya kuiga kitu kizuri. Tanzania ukishapita mitaa miwili mitatu watu wanakugeuzia shingo na kukuita jina basi unaona umeshamaliza kila kitu na unaridhika kabisa.

Kwa wenzetu mastar wakubwa kila wanachokifanya ni habari na wanaelewa kwamba ile ndio Price of being a superstar, sasa nyinyi kuongelewa filamu tena mara nyingine hata hujaskiliza wewe umefanya tu kuletewa tu habari “INDIRECT SPEECH” ambayo maranyingi kama sio zote haifiki kama ilivyokuwa ndio mnajipanikisha hivyo na mishipa inawasimama. Tutafika kweli? hakuna kitu kibaya kama umasikini wa mawazo/akili, ni bora umasikini wa mali.

Kiukweli mnasikitisha sana na mko kwenye hali mbaya mno bila nyinyi wenyewe kujijua. Acha wanaoendelea kuwasifia ujinga wawasifie na endeleeni kujazana ujinga ila mkikutana na WENZENU wa nchi nyingine ndio mtajiona MKO NYUMA kiasi gani, mara nyingi huwa tunapwaya.
Kibongobongo mtapeta lakini kama lengo ni kufika Hollywood kama mnavyokuwa mnajibu kwenye interview zenu kwa hali hiyo ya kutotaka mabadiliko MNAJIDANGANYA.

Katika maisha yangu mimi ni mtu ambae huwa napenda sana ukweli hata kama utaniuma na sipendi kuukimbia ukweli hata siku moja, acha uniume lakini nijifunze kutokana na huohuo ukweli, tuepuke kuwa wapumbavu, bora tuwe wajinga kwasababu tutajifunza na tutaerevuka, hakuna aliezaliwa anajua, yote tumeyakuta duniani na tunaendelea kujifunza kadri siku zinavyokwenda mbele.

Mwenye masikio na asikie mwenye macho na aone, ni mawazo yangu tu si lazima ukubaliane nayo na hayahusiani na mtu yoyote.

Asante
Zamaradi Mketema.

FIESTA MOSHI IMETISHA...

Fiesta Moshi hainaga majotro.. wananchi wakijiachia!!!

Wednesday, July 13, 2011

BREAKING NEWS: MBUNGE WA IGUNGA ROSTAM AZIZ AJIUZULU LEO.. WATU WAONESHA KUTOKUKUBALIANA NA KUPINGA MAAMUZI HAYO.

Mbunge wa Igunga na mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi NEC kupitia mkoa wa Tabora Rostam Aziz siku hii ya leo kwa ridhaa yake ametangaza kujiuzulu na kuachia ngazi katika nyadhifa zote alizokuwa nazo kama mjumbe wa Nec na Mbunge wa igunga,

Tamko hilo amelitoa siku hii ya leo majira ya saa tisa alasiri katika Ukumbi wa Sakao huko Igunga tabora...

Baada tu ya kutoa Tamko hilo wananchi waliokuwa eneo hilo walionekana kutoridhishwa kabisa na maamuzi hayo yaliyotolewa na kuonekana wazi kabisa wakipinga huku wakisema 'HATUTAKI" wakipinga uamuzi huo uliotolewa kwa kumtaka aendelee kuwepo kwenye nyadhifa hizo ambapo mbali na kuwa Mbunge pia alikuwa mjumbe wa NEC.


Rostam alikuwa ni mbunge wa IGUNGA kwa vipindi vinne mfululizo na alikuwa ni mjumbe wa NEC kwa Awamu tatu.

PICHA MSETO... HAPA NA PALE



HAPO nikiwa na Barbara Hassan wa Power breakfast ya CLOUDS FM, hizi zilikuwa ni shamrashamra za Fiesta katika jiji la Mwanza ambapo tulikuwa tukizunguka mitaa tofautitofauti. Madereva walikuwa makini sana kusikiliza kinachoongelewa ili waweze kujibu maswali maana kilichokuwa kinaendelea ni Ugawaji wa mafuta ya BURE kabisa kutoka katika moja ya makampuni ambayo ni wadhamini wa Fiesta pia kwenye swala la usafiri wa ardhini GAPCO.
Hapo T-shirt ndio zilikuwa mpango.. mtu anaweza hata akakuvamia ili tu apate T-shirt za Fiesta.. watu wana mapenzi na fiesta mpaka basi aisee...
Nikiwa nafanya LIVE katika jiji la MWANZA kwa kushirikiana na Adam mchomvu ambae tulikuwa nae huko pia!!! Adam Mchomvu nae ndie huyo katika Live ambayo tulikuwa tukishirikiana..
Sijui nilikuwa naambiwa nini, hata sikumbuki lakini itakuwa kuna jambo nilikuwa nakumbushwa na Barbara Hassan. Hii ilikuwa ni LIVE kutoka Uwanjani.. Zamaradi, Adam pamoja na Reuben Ndege (Ncha kali)

HAPPY BIRTHDAY SHADEE...

Anaitwa Saida Khalfan a.k.a Sade (shadeiyaaa) mtangazaji wa CLOUD 9 kupitia Clouds Tv, leo ni siku yake kubwa sana kwenye maisha yake sababu ni siku yake ya kuzaliwa hivyo nachukua nafasi hii kumtakia kila la kheri katika siku yake hii kubwa na katika maisha yake kwa ujumla!!!
HAPPY BIRTHDAY TO YOU!!!

WAKILISHA MIAKA HAMSINI YA UHURU!!!!

Hizo T-shirt unazoona tumetupia ni Design ya Ally Rhemtullah pamoja na Vida mahimbo zikiwakilisha miaka 50 ya Uhuru.. hapo niko na Jimmy jam pamoja na mbunifu Ally Rhemtullah!!
Hii ilikuwa ni MWANZA kama tulivyo juu na pembeni ameongezeka Albert G. Sengo mwenye T-shirt Nyeusi ambae huwa ni mwenyeji wetu kutoka Mwanza.



Zinapatikana kwenye rangi tofautitofauti kama Nyeusi, Nyeupe, Nyekundu kama unahitaji unaweza kuwasiliana na Ally ama Vida ambao ndio madesigner wa T-shirt hizo!!!

Monday, July 11, 2011

NIMEJIKUTA NIMEMPENDA TU HUYU MSICHANA...

Nimeiona hii picha ya huyu model kutoka kwa Nuru the light, nikajikuta nimempenda tu huyu msichana bila sababu ya msingi..

Pamoja na kwamba walikuwa ma-model wengi lakini nilijikuta jicho langu limeganda hapa...

To me she is really Beautiful.. nimempenda tu na sina sababu ya msingi.. hivyo sio mbaya hiyo ikawa picha ya leo!!!

MJENGONI LEO HII...

Ndio tulivyoianza jumatatu kinamna hiyo... Zamaradi Mjengoni leo!!!
Antu na Zamaradi

Kutoka kushoto ANTU ambae utampata soon kupitia Clouds TV, ZAMARADI pamoja na mama wa ng'aring'ari SAKINA WA LYOKA!!!
Babuu wa kitaa pamoja na Antu
Ceaser Daniel
Kama tulivyo hapo juu, Antu, zamaradi, sakina
With my girl Antu Mandoza...
Sakina Lyoka na Antu.. YANGA OYEEEEEEEEEEEEE
Hapo nikiwa na mamaa wa ng'aring'ari....

Hizo ndio picha za mjengoni jumatatu ya leo!!!

NIMEMALIZA!!!

VOTE FOR HEMEDY...






Muigizaji na muimbaji kutoka Tanzania HEMEDY SULEIMAN (PHD) yuko kwenye Tusker project Fame (Tusker all stars) kwasasa... ili aweze kushinda anahitaji sana kura yako Mtanzania, piga kura yako sasa..
Hapo akiwa na Desmond Elliot kutoka Nigeria



Ili kumpigia kura Hemedy andika TUSKER 3 kwenda namba 15324

KUTANA NA WATOTO WA SOLO THANG...

Huyo hapo juu ni mwanamziki wa siku nyingi Solo thang ambae alitamba kwenye nyimbo tofautitofauti kama vile MTAZAMO alioshirikiana na afande sele, KAMA UNATAKA DEMU ambayo alishirikiana na Jaymoe, MAMBO YA PWANI ambayo aliimba yeye mwenyewe na nyingine nyingi sana...


hajasikika kwa muda mrefu sana ila kwasasa yuko nje ya nchi ambapo ana familia yenye watoto wawili wazuri sana kama unavyowaona, na anastahili pongezi kwa hilo!!!


Hapa Solo thang akiwa na watoto wake wawili, wa kwanza ni huyo wa kiume anaitwa Yassir (4) na wa pili ni wa kike anaitwa Zaynab mwenye miaka miwili na nusu


Father and Son.. huyo ni mtoto wake wa kiume anaitwa YASSER
Na hiki ndio kifaa chake, mtoto wake wa kike anaitwa Zaynab, veery beautiful kwakweli!!!
Watoto wake kwenye picha ya pamoja!!!!
Mh!!! look at those eyes... aisee nafkiri picha inaeleza kilakitu... sooo CUTE!!!

Father and daughter!!!

kako so sweet...

Huyo ndio Solo thang na hayo ndio maisha yake kwasasa ambapo ni baba wa watoto wawili hao unaowaona hapo juu..


HONGERA SANA AISEE!!!!

Saturday, July 9, 2011

JACKY WOLPER ATAKA KUZICHAPA NA RAIS WA SHIRIKISHO...

Katika hali isiyotegemewa na mtu yeyote siku ya jana kwenye kikao kilichoandaliwa na shirikisho la wasanii Tanzania TAFF chini ya Rais Simon Mwakifamba na kuhudhuriwa na wadau pamoja na wasanii mbalimbali, msanii wa filamu Jackline Wolper Massawe alitaka kulianzisha na kuchafua utaratibu mzima wakati Rais wa shirikisho akiendedlea kuhutubia ambapo Jacky alijikuta akichomoka alipokuwa amekaa na kuelekea jukwaa kuu kwa lengo la kumvamia rais wa shirikisho la filamu Tanzania Simon Mwakifamba.

Hali hiyo ilijitokeza baada ya Rais huyo kutoa ushahidi wa magazeti tofautitofauti unaoelezea skendo mbalimbali za wasanii na mmonyoko wa maadili ndani ya industry ya filamu kitu ambacho inasemekana kilimkera Wolper kwa kuona rais ni kama anawagandamiza badala ya kuwatetea wasanii wake, hivyo akaona njia pekee ni kumdiscipline rais huyo kwa kutaka kumvamia pale jukwaani alipokuwa.

Zoezi lake hilo la uvamizi halikuweza kufanikiwa kwani alijikuta akitaitiwa na mabaunsa waliokuwa standby kwa ajili ya kazi hiyo na hivyo kuzima harakati zake hizo za uvamizi katika jukwaa hilo ambalo lilisheheni viongozi tofautitofauti wa shirikisho la filamu.

Juhudi za kumtafuta jacky pamoja na Mwakifamba zinaendelea ili waweze kuongelea swala hili kwamba ilikuwaje..
Hiyo ndio hali ilivyo kwasasa kwenye industry ya filamu ambapo kiukweli kumeibuka makundi makubwa mawili ambayo yanapigana vita usiku na mchana, moja likiwa chini ya shirikisho la filamu Tanzania na lingine likiwa ni Bongo movie FC ambao mara nyingi hujihusisha na mambo ya mipira, hivyo shirikisho kupata wasiwasi juu ya uibukaji wa kundi hili jipya kwa kuona kuna kama shirikisho lingine chini ya viongozi wengine ambao sio rasmi hivyo kuhofia kutotambulika kwa shirikisho lenyewe..

NINACHOWAZA hivi jacky angefanikiwa kufika pale ingekuwaje!? Angepigana ama vipi?? na katika kupigana huko angeweza kweli kuzikinga na mwanaume yule!!?? na hata kama angeweza ile ndio Ilikuwa SOLUTION hata kama wanaonewa!?? ama labda alikuwa anafanywa chambo!!?? hayo ni baadhi tu ya maswali ninayojiuliza mimi binafsi ambayo hayahusiani na chochote kile wala upande wowote ule, mwisho wa siku waarabu wa pemba wajuana kwa vilemba bwana kazi yangu ni kukuhabarisha tu ya mjini..
YA NGOSWE MUACHIE NGOSWE!!!

HATUNA CHA KUFICHA SABABU MAPENZI YETU NI YA UKWELI NA HATUACHANI KAMWE - DIAMOND NA WEMA.... EXCLUSIVE PHOTOS!!!!!

Diamond na Wema.. Mahaba Moto kama unavyowaona!!!
Hayo ni maneno yaliyotamkwa na wapenzi hao wawili Diamond na Wema na kusema kwamba pamoja na kwamba watu wanaongea sana juu yao, wao wawili hawajali maneno ya watu na wala hawategemei kuachana leo wala kesho kwani wanapendana sana hivyo maneno ya watu hayataathiri chochote kwenye mapenzi yao..


Na kingine walichozungumzia ni uwazi wa mapenzi yao na kusema hawaoni sababu yoyote ya kuficha chochote kile sababu wanajiamini na mapenzi yao sio ya kubabaisha ila ni ya dhati kutoka mioyoni mwao so wapambe mliokuwa mkihoji juu ya kuachana kwao habari ndio hiyo..
WEMA and DIAMOND kama unavyowaona..
DW forever...... MPO!!??

Hizo ni baadhi tu ya Exclusive photos kutoka kwa blog hii Pekee, kwa nyingine zaidi na zaidi endelea kupitia humu nitakushushia soon!!


Stay tuned....