
Kama una kumbukumbu nzuri huenda umeshaiona hii sura zamani kidogo enzi hizo kwenye tamthilia ya kaole ambapo alikuwa akitambulika kama Mr. DIMERA, lakini jina halisi ni SIMON SIMALENGA ambapo kwa sasa ameachana na mambo ya maigizo na yuko hapa CLOUDS FM RADIO kama PRODUCER wa vipindi vya NJIAPANDA pamoja na JAHAZI ingawa pia hufanya na vipindi vingine lakini pia ni Mwanafunzi wa MWL NYERERE MEMORIAL ACADEMY ambapo anachukua Bachelor in POLITICS.

Alizaliwa miaka 35 iliyopita huko Njombe mkoa wa IRINGA, na elimu yake ya msingi aliipatia Tengero priamry School huko Morogoro Vijijini wilaya ya Mgeta na hiyo ilikuwa 1987 - 1993.
Baada ya hapo alipumzika kidogo mpaka mwaka 2004 alivyokuja kujiendeleza kwa kufanya Special Programs kama Private Candidate ambapo alisoma miaka miwili kwa minne.. Na baada ya hapo alichukua ADVANCE CERTIFICATE in Journalism na kisha akachukua DIPLOMA in JOURNALISM na kisha akajikuta ameingia kwenye sanaa mpaka alipokuja kuacha na kujunga na Tasnia ya Habari...
QN: TOFAUTI YA KAZI YAKE YA ZAMANI(MAIGIZO) NA YA SASA NI NINI??
ANS: Wakati nafanya maigizo nilikuwa na malengo ya kuwafikia baadhi ya watu (kiserikali na kijamii) na kwa kipindi hiko ilikuwa ni vigumu ingawa hao watu niliotaka kuwafikia huenda wao walikuwa wakiniona kutokana na kazi yangu(maigizo) ila mimi ilikuwa ni vigumu kwa upande wangu kuwafikia, LAKINI kwasasa imekuwa rahisi kuwafikia kutokana na kazi ninayofanya ingawa vyote hivi navifanya kwa malengo fulani, kwani bado kabisa sijafika ninapotaka kufika na ili niweze kufika ninapopataka hatua nyingine niliyofanya ni kurudi shule ambapo kwasasa nasoma MWL JK NYERERE MEMORIAL kama nilivyosema awali.
QN: MALENGO YAKO NI NINI HASA!!??
ANS: Malengo yangu hasa ni kuwa MWANASIASA, na ninaposema mwanasiasa si uanasiasa tu, ila mwanasasa mwenye nia ya dhati ya kutekeleza kile ninachokiona kina upungufu kwenye jamii.

QN: WEWE NI MTU WA AINA GANI!??
ANS: Kwakweli mi ni mtu ambae kwenye Starehe SIPO KABISA, na hata ukisikia kuna wimbo umetoka mpya halafu mi naujua basi ujue huo wimbo ni Mzuri kwelikweli maana mi si mfatiliaji kabisa wa hayo mambo.. Na pia napenda kufatilia nmustakabali wa taifa letu na nini kinaendelea kitaifa hata kama ni kidogo hakiwezi kunipita, ingawa kitu kingine ambacho napenda kidogo labda MOVIES, tena aina ya movies ninazopenda ni zile za KIPELELEZI.
QN: NI NINI UNACHUKIA!!??
ANS: Nachukia sana mtu kutokua serious, sipendi mtu ambae ana mzaha mzaha mwingi, mtu ambae hayuko makini, anaamka hata hajui nini kilitokea jana kiufupi huwezi kunikuta karibu na mtu wa aina hiyo, mtu ambae hayuko Current.
QN: NI KITU GANI MUHIMU SANA KATIKA MAISHA YAKO!??
ANS: Nchi yangu na watu wake.
QN: KITU GANI CHA AJABU ALICHOWAHI KUFANYA NA HUENDA ANAKIJUTIA!!??
ANS: Kupata Mtoto Nje ya Ndoa, hiko ndio kitu ninachojutia ingawa haina maana kwamba simpendi mtoto wangu, nampenda sana ila tu SIKUPLAN.
QN: Tofauti ya kazi yake ya zamani(maigizo) na sasa ni nini!??
ANS: Wakati nafanya maigizo nilikuwa na malengo ya kuwafikia baadhi ya watu (kiserikali na kijamii) na kwa kipindi hiko ilikuwa ni vigumu ingawa hao watu niliotaka kuwafikia huenda wao walikuwa wakiniona kutokana na kazi yangu(maigizo) ila mimi ilikuwa ni vigumu kwa upande wangu kuwafikia, LAKINI kwasasa imekuwa rahisi kuwafikia kutokana na kazi ninayofanya ingawa vyote hivi navifanya kwa malengo fulani, kwani bado kabisa sijafika ninapotaka kufika na ili niweze kufika ninapopataka hatua nyingine niliyofanya ni kurudi shule ambapo kwasasa nasoma MWL JK NYERERE MEMORIAL kama nilivyosema awali.
QN: MALENGO YAKO NI NINI HASA!!??
ANS: Malengo yangu hasa ni kuwa MWANASIASA, na ninaposema mwanasiasa si uanasiasa tu, ila mwanasasa mwenye nia ya dhati ya kutekeleza kile ninachokiona kina upungufu kwenye jamii.
QN: WEWE NI MTU WA AINA GANI!??
ANS: Kwakweli mi ni mtu ambae kwenye Starehe SIPO KABISA, na hata ukisikia kuna wimbo umetoka mpya halafu mi naujua basi ujue huo wimbo ni Mzuri kwelikweli maana mi si mfatiliaji kabisa wa hayo mambo.. Na pia napenda kufatilia nmustakabali wa taifa letu na nini kinaendelea kitaifa hata kama ni kidogo hakiwezi kunipita, ingawa kitu kingine ambacho napenda kidogo labda MOVIES, tena aina ya movies ninazopenda ni zile za KIPELELEZI.
QN: NI NINI UNACHUKIA!!??
ANS: Nachukia sana mtu kutokua serious, sipendi mtu ambae ana mzaha mzaha mwingi, mtu ambae hayuko makini, anaamka hata hajui nini kilitokea jana kiufupi huwezi kunikuta karibu na mtu wa aina hiyo, mtu ambae hayuko Current.
QN: NI KITU GANI MUHIMU SANA KATIKA MAISHA YAKO!??
ANS: Nchi yangu na watu wake.
QN: KITU GANI CHA AJABU ALICHOWAHI KUFANYA NA HUENDA ANAKIJUTIA!!??
ANS: Kupata Mtoto Nje ya Ndoa, hiko ndio kitu ninachojutia ingawa haina maana kwamba simpendi mtoto wangu, nampenda sana ila tu SIKUPANGA kupata mtoto.
QN: NI NINI UNATAMANI KUULIZWA NA HUJAWAHI KUULIZWA POPOTE!!??
ANS: Ni kuhusu SIKU YANGU YA KUZALIWA, Sijawahi kuulizwa na mtu ninajisikiaje ikifika siku yangu ya kuzaliwa... Kiukweli kabisa SIJAWAHI KUJISIKIA VIZURI kwenye siku yangu ya kuzaliwa, sababu inaweza ikawa ya kipuuzi lakini kwangu ni ya msingi, Kwanza kabisa naona muda unakwenda hivyo najihisi nina deni na changamoto kubwa sana kwa jamii ya kitanzania kwani mimi kama kijana najihisi sijatoa mchango kwa kiasi cha kutosha hata kwa jamii inayonizunguka, hiyo ndio sababu kubwa.
QN: KITU GANI HATUJUI KUTOKA KWAKO??
ANS: Sijawahi kufanya Birthday katika maisha yangu na wala sitegemei.
QN: KINGINE TUSICHOKIJUA??
ANS: Kuna mtu ananipa Tabu sana kwenye maisha yangu, na huyu si mwingine ila ni Muheshimiwa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, JAKAYA MRISHO KIKWETE, na kikubwa kinachonipa tabu kutoka kwa huyu mtu ni kwamba huwa natamani sana kujua kama ningekuwa na uwezo ningeweza kuingia kwenye kichwa chake ili nione tu muda wote NI NINI AMBACHO HUWA ANAFIKIRIA AMA KUWAZA, natamani sana kujua muheshimiwa rais huwa anawaza nini na pia nijue ni Mtu wa aina gani sababu huwa anabadilikabadilika sana, mara nyingine huwa charming na mara nyingine huwa tofauti kabisa, na nashkuru kwa mwaka huu nimepata bahati ya kuonana nae zaidi ya mara tatu lakini bado kuna kitu huwa kinanipa tabu sana juu yake sababu sijawahi kuongea ambacho ninacho kwenye kichwa changu (ninachotaka/tamani kumwambia).

QN: NANI ANAKU-INSPIRE??
ANS: Mh. Jakaya Mrisho Kikwete huwa anani-insipire sana, naweza nikasema hata kurudi kwangu shule kumechangiwa kwa kiasi kikubwa sana na yeye, na ilikuwa nisomee sheria lakini nikaona nikisomea sheria itakuwa ngumu sana kumfikia hivyo nikaona nisomee habari na kwa kupitia hilo nashukuru nimeweza kuonana nae zaidi ya mara tatu kwa mwaka jana ingawa sijawahi kuongea ambacho ninacho kwenye kichwa changu.
QN: TOFAUTI YA ALICHOKUWA AKIKIFANYA ZAMANI NA SASA??
ANS: Zamani nilipokuwa kwenye maigizo ilikuwa tunatumia kipaji lakini ilikuwa ngumu sana kutumia akili yako kuweka ubunifu.. mambo mengi yalikuwa yanaendeshwa na kipaji zaidi na hiyo ilitokana na watu waliokuwa wakinizunguka, lakini kwasasa angalau kati ya ASILIMIA 100 angalau natumia hata 45% ya ubongo wangu katika kufanya mambo tofautitofauti, na hata sehemu ninayofanyia kazi inanipa uhuru wa mimi kufanya kazi yangu vizuri na haikulimit katika kufikiria. na kizuri zaidi kinachonifurahisha nina uhuru hata wa kujiendeleza kielimu tofauti na makampuni mengine ambayo ukisema unaenda kusoma basi ni kama umejifukuzisha kazi mwenyewe.
QN: KATIKA WATU WOTE ALIOWAHI KUWAHOJI, NI WATU GANI ALIFURAHI SANA KUHOJIANA NAO??
ANS: Mheshimiwa Rais JAKAYA MRISHO KIKWETE, Profesa ANA TIBAIJUKA, pamoja na WAZIRI WA MAMBO YA NJE mh. BENARD MEMBE.
QN: MWISHO KABISA UNA CHOCHOTE CHA KUONGEA??
ANS: HUWA NAKERWA SANA na Baadhi ya MAWAZIRI, MANAIBU na MAKATIBU WAKUU WA WIZARA mbalimbali ambao hufanya baadhi ya taarifa za kiserikali kuwa SIRI.. wakati mara nyingi ninapotaka mahojiano nao huwa ni kwa nia njema na kwa maslahi ya taifa