Monday, June 14, 2010

MWANAMKE UREMBO - USIONE VYAELEA

NILIMBAMBA KEISHA SALON MOJA AKIJIWEKA SAWA
Nilimkuta Keisha salon moja hivi akijitayarisha kwa ajili ya Graduation yake ya kumaliza Form Six inayofanyika leo pale Laureate international school, hapa akiwa anatengenezwa nyusi

HAIR DO - BEFORE
hapa kabla haijamaliziwa style yake ya nywele ilikuwa ikionekana hivi

Hapa weaving likishashonewa linakatwa kistyle ili kitokee kitu kizuri

Mambo ya Sandra hayo kama unavyomuona.. Busy mwenyewe akimuweka sawa mdada

HAIR DO - AFTER

Hapa ndio mambo yamemalizika kwa nyuma inaonekana hivyo

Kwambele ndio kama unavyoiona

hapo mdada ameshapendeza.. Mwanamke Urembo

Friday, June 11, 2010

HAMMA Q ANENA BAADA YA KUTOKA JELA


Inawezekana ulikuwa hulifahamu hili lakini habari ni kwamba Mwimbaji wa PEMBE LA NG'OMBE kutoka bendi ya Dar Modern Taarab ambapo hapo awali alikuwa ni mwanamuziki wa bongo Flavour HAMA Q ameipata joto ya rumande alikokuwa under arrest katika Gereza la Keko hapa DSM kwa muda wa wiki kadhaa na ameachiwa kutoka Gereza la KEKO mwezi uliopita mwishoni kama kwenye tarehe 29 may (kama sikosei). Ambapo kesi iliyokuwa ikimkabili ni kujeruhi.

Akiwa katika studio za clouds fm leo katika leo tena

katika mahojiano leo Hamma Q ametoa hali halisi ya jinsi jela kulivyo ambapo amesema kwamba mtindo wa kulala ni ubavu ubavu na si chali wala kifudifudi ili usichukue nafasi kubwa, na ukitoka tu kwenda kujisaidia nafasi yako imechukuliwa.


Amesema alipokuwa huko amejifunza mambo mengi sana lakini kubwa ni swala zima la kubana matumizi ambapo chupa ya maji inaweza kutumiwa hata kwa siku mbili, na si kubana matumizi kwenye vyakula tu bali hata karatasi ambazo huwa wanatumia kuandika ujumbe na kuutuma kwa ndugu na jamaa zao.. kipande cha karatasi moja anaweza akakitumia hata zaidi ya mara kumi.

Na huko jela kumbe biashara ya kubadilishana bidhaa kwa bidhaa ambayo ilikuwa ikitumika zama za zamani bado inaendelea ambapo ukiletewa chakula unaweza ukabadilishana na mtu kwa chupa ya maji..

hayo ndio maisha ya huko ndani ambapo yeye anasema siku moja jela ni kama mwaka hakuna uzuri kabisa ila anashukuru alivyofika huko kujulikana kwake kulimsaidia kidogo AKASALIMIKA.. masela hawakumsumbua kwa chochote mpaka anaaga jengo hilo lisilokuwa na heri.

Hii sio mara ya kwanza kwa Mastar wetu hapa Tanzania kuonja joto ya rumande ama jela, ukiachana na Wajelajela (FM Academia) ambao wao waliitungia hadi nyimbo JELA, Mtu wa kwanza katika muziki wa kizazi kipya kushtua watu kwamba jela ipo alikuwa ni Khaleed Mohammed (TID) ambae alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kabla ya kupata msamaha.. Na wengine waliokumbwa na zahma hiyo ni pamoja na Actress mwenye jina kubwa aliewahi kuwa miss Tanzania Wema sepetu, Miss tanzania 2009 Miriam Gerald, Mwimbaji wa bendi Waziri sonyo na wengineo wengi...

Kwasasa Hama Q ametoa wimbo wake mpya kabisa unaoitwa toto la kiafrika akiwa na bendi yake ya DAR MODERN TAARAB.. hatujui kama utakuwa kama Pembe la ng'ombe ama vipi!!

MAMBO YA MISS DAR INDIAN OCEAN..

Mrembo aliefanikiwa kunyakua taji la Miss Dar Indian Ocean Usiku wa jana ALICE LUSHIKO
TATU BORA ya Miss Dar Indian Ocean

Hii ndio TOP FIVE ya Miss Dar Indian Ocean (mrembo mwenye nambari 13 ndie aliechukua taji)

Kabla ya top 5 kulikuwa na NANE BORA ambayo ndio hiyo kama unavyoiona.

Meza ya Majaji kutoka kushoto BOY GEORGE, MANGE KIMAMBI, KISA na GERALD HANDO ambae ndio alitangaza washindi.


HAPA CHINI NI BAADHI YA WAHUDHURIAJI

Waandaji wa mtanange huo (Frontline management) Nancy sumari (kushoto) pamoja na Irene Kiwia
Jokate Mwegelo

Huyu ni mshiriki ambae ataiwakilisha wilaya ya Temeke

Irene kiwia (kulia) akiwa na mdadaa

Shamim zeze (8020)

Kutoka kushoto Arnold Kayanda, Rommy Jones pamoja na Ali Model (Daxx)

Vijana nao walikuwepo kushuhudia warembo.. Nas tatu

Nikiwa na Brothers.. Ze Boy (THT) kushoto kwangu, Moracka kulia pamoja na Martin anaechungulia kwa juu hapo

nikiwa na Jokate

Nancy Sumari

Martin mvuto kwanza, Ali Daxx pamoja na Rommy Jones

Nikiwa na vijana wa mjengoni (ukikaa nao hawa unacheka tu muda wote)

Thursday, June 10, 2010

USINIZINGUE...............

Hiyo picha ni kama inaongea hivyo.. hata mimi naziweza!!

BI KIDUDE akiwa na Geah habib katika utani wa hapa na pale na wajukuu zake.

Ukipata bahati ya kukaa na bi kidude hutanuna hata sekunde moja, ni mtu anaefurahisha sana kwa waliobahatika kukaa nae watakiri kitu hiko.. anachekesha mno!!!

ZAWADI KUTOKA KWA ANKAL MISUPU

Nikiwa na Shamsa Ford na zawadi zetu (zawadi ni zawadi) kutoka kwa ankal michuzi shukrani sana.
Shamsa ford na zawadi yake


Wednesday, June 9, 2010

UNAMJUA HUYU!!!?????

Habari yako bwana..!!!!!

Unamjua huyu!!?? Umeshawahi kumuona sehemu??? kama unamjua nataka uniambie umemuona wapi!? ama kwenye nini?? Na si vibaya kama una jina lake na mi unitupie nilijue...

HAPPY BIRTHDAY BIG BOSS

Leo siku ya tarehe 9th June ndio kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa ya Managing director wa CLOUDS fm Mr. Joseph Kussaga.. HAPPY BIRTHDAY TO YOU!!!
Ze cake



Ilikuwa kama suprise kwake yeye hakujua kinachoendelea... Hapo juu ni baadhi ya wafanyakazi wa Clouds Entertainment wakimpongeza!!!

Tuesday, June 8, 2010

NILIYOYASHUHUDIA KWENYE MECHI YA BRAZIL na TAIFA STARS

Katika hali ya kawaida Mechi kati ya Brazil na Taifa stars ni kitu kikubwa sana, na hiyo yote inatokana na ukubwa wa timu yenyewe.
Kutokana na ukubwa wa timu Magoli matano tuliyofungwa inaweza ikawa sio habari pia kwasababu ni kitu ambacho kilikuwa kinategemewa kutokana na ukubwa na uzoefu wa timu yenyewe tuliokuwa tukicheza nayo.
Lakini kuna matukio mengi ambayo yalitokea jana na ndio hayo yanayoweza kuwa habari kwenye mechi ya jana

La kwanza ni yule kijana wa kitanzania alieruka Fence na kuvamia uwanjani kabisa wakati mpira ukiendelea na moja kwa moja kwenda kumkumbatia mchezaji wa Brazil KAKA ambae nae alimpa ushirikiano wa kutosha tu kwenye hilo(HUKU MPIRA UKIENDELEA) na baada ya hapo akatoka uwanjani akiwa na Furaha ya ajabu ila wazee wa kazi wakamtight lakini lengo lake likiwa limeshatimia. Ni kitu ambacho hakijawahi kutokea!!

Tukio lingine ni lile lililomhusisha mchezaji wa Taifa stars JERRY TEGETE pamoja na mchezaji wa timu ya taifa ya Brazil (Defensive midfielder) GILBERTO SILVA.Mara nyingi wachezaji wanapomaliza mchezo huwa na kawaida ya kubadilishana jezi na hata kwenye mchezo wa jana pia ilikuwa hivyo ambapo baada ya mchezo SILVA na TEGETE walionekana kubadilishana jezi lakini kilichotokea ni kwamba baada ya TEGETE kupokea jezi ya mchezaji huyo wa Brazil na yeye akavua yake ili amkabidhi mchezaji huyo wa Brazil ila katika hali isiyotegemewa na wengi GILBERTO SILVA ALIIKATAA jezi ya Tegete na kuondoka huku akiwa amemuachia jezi yake, kitendo ambacho kila mtu alieshuhudia alikitafsiri katika hali yake.

Wakati wimbo wa taifa wa Brazil unaendelea kuna sauti nyingine zilikuwa zinasikika kupitia Spika zilezile za pale uwanjani na kusababisha muingiliano wa vitu hivyo.

Wimbo wa taifa wa TANZANIA mara ya kwanza ulikuwa ukikatika katika na kusababishwa urudiwe tena kwa mara ya pili ambapo ndio ulikubali kucheza vizuri.

WEWE UMEONA NINI KWENYE MECHI HIYO???

CLOUDS MEDIA GROUP IMETOKA MBALI....!!!

Mabosi zetu enzi hizo za mwalimu.. JOSEPH KUSSAGA(kushoto) na RUGE MUTAHABA (kulia) (wadogooo) wakiwa na DJ MIND MOTION (katikati) wakati huo alikuwa ni NUMBER ONE DJ wa SAN FRANSISCO, hapo ilikuwa ni MAREKANI mwaka 1998.

Kila kwenye mafanikio kuna mwanzo wake.. Focus is everything in life.. hapo Bosi wetu JOSEPH KUSSAGA akiwa mitamboni.. ulikuwa kama ni mwanzo tu wa safari ambao ndio umesababisha CLOUDS unayoiskia sasahivi.

Kutoka kushoto JOSEPH KUSSAGA (mwenye shati la blue), BONNY LUV, wadada wawili ambao majina yao sikufanikiwa kuyapata, RUGE MUTAHABA mwenye shati ya brown na kwa huko juu kutoka kushoto ni DAUDI LEMBUYA na OTHMAN NJAIDI.

Vichwa vilivyoifanya Clouds ifike hapa ilipo.. RUGE MUTAHABA(katikati) na JOSEPH KUSSAGA (kulia).. wakiwa na Dj Mind Motion the number ONE Dj wa enzi hizo huko San fransisco.

Penye nia pana njia... Kutoka Disco la kawaida mpaka kumiliki Radio ambayo ni TALK OF THE TOWN and THE HOTTEST RADIO STATION in Tanzania CLOUDS FM, CLOUDS TV, CHOICE FM, COCONUT FM -Zanzibar, PRIME TIME PROMOTIONS pamoja na kutoa MCHANGO mkubwa sana kwenye Entertainment industry ya Tanzania na mafanikio mengine mengi.

SALUTE!!!!

HATIMAE MTU NINAEMJUA AKWEA PIPA...

Kuna hii promotion inayoendelea ya 'KWEA PIPA NA COCA COLA' ambayo inahusisha zawadi ya kwenda South Africa kushuhudia kombe la dunia...
Leo hapa ofisini kwa macho yangu nimeshuhudia mtu ninaemjua akifungua kisoda na kukuta hali hiyo unayoiona ambayo ndio zawadi kubwa (Ticket ya kwenda south Africa kushuhudia Kombe la dunia).
Kwahiyo inadhihirisha kabisa zawadi zipo, endelea kunywa soda halafu ufungue kizibo unaweza ukawa mshindi mwingine.

JIDE - A TRUE DIVA.. I LOVE THIS WOMAN!!

Anaitwa Judith wambura Mbibo.. The Wife of Captain Gadna G. Habash, ukiniuliza sababu kwanini nampenda huyu mtu naweza nikawa sina Strong reason lakini ni mmoja kati ya watu wanaoni-INSPIRE sana hapa Tanzania.
Hapa nikiwa katika moja ya show zake..

Kutoka kushoto JOAN, lady jaydee katikati pamoja na mimi hapo pembeni.

YALIKUWA NI MAPENZI TU....

Katika maisha inaweza ikatokea ukampenda mtu mpaka ukawa na uwezo wa kufanya chochote kwa ajili yake.. When it comes to Celebrities inaweza ikatokea ukampenda Celebrity fulani aidha mwanamuziki, muigizaji, mtangazaji, mcheza mpira ama yoyote tu kiasi kwamba kwako kushikana mkono tu na yeye inakuwa ni KITU KIKUBWA kuliko chochote.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja wa TANZANIA aliruka Fence na kwenda kumkumbatia mchezaji wa Brazil KAKA na kisha kuondoka akiwa na furaha ya ajabu.

lakini baadae mapolisi walimtia nguvuni na kuanza kumpa kichapo kitu ambacho naona kama sio sawa.. nafkiri wangemkamata tu na kumuweka chini ya ulinzi kisha kufata sheria jinsi ilivyotaka na si kichapo kile alichopewa.
THAT WAS LOVE kwa mchezaji huyo wa Brazil na kwake yeye jana ilikuwa ni kama kutimiza moja ya NDOTO ZAKE za muda mrefu..

Inasemekana kwamba kijana huyo ni Mtanzania anaeishi south Africa na alitoka South Africa kuja Tanzania maalum kwa ajili ya kushuhudia mechi hiyo ya BRAZIL na TAIFA STARS

Thursday, June 3, 2010

FASHION FOR EDUCATION NDANI YA JAHAZI LEO

Nancy Sumari (Mratibu) akiwa na Ally Rhemtulla ambae ni mbunifu wa mavazi katika show ya Fashion for education.. ambayo ni FASHION show kwa ajili ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia shule za sekondari Tanzania.
Hapa wakiwa na CAPTAIN Gadna G. Habash ndani ya studio za Clouds FM leo katika kipindi cha JAHAZI

Onesho hili litafanyika jumamosi hii ya tarehe 5 June 2010 katika hoteli ya DOUBLE TREE by Hilton pale Masaki kwa kiingilio cha 50,000/- tu

Hii ilikuwa ni LEO ndani ya JAHAZI la Captaiin kama unavyomuona pichani akiwa na NANCY pamoja na ALLY RHEMTULLAH.

BELIEVE IN YOURSELF

If you believe
Within your heart
You’ll know that no one can change
The path that you must go
Believe what you feel
And know you’re right because
The time will come around
When you’ll say it’s yours

Believe that you can go home
Believe you can float on air
Then click your heels three times
If you believe
Then you’ll be there
That’s why I want you to
Believe in yourself
Right from the start
Believe in the magic
Right there in your heart
Go ahead believe all these things
Not because I told you to
But believe in yourself
If you believe in yourself
Just believe in yourself
As I believe in you


(charlie smalls)

Can dreams dream?


A dream can dream a wonderful thing.

A dream can dream a horrible thing.

A dream can dream fantastic things.

A dream can dream a sad thing.

A dream can dream happy things.

A dream can dream a lonely thing.

But, most of all, Dreams can dream!

MKONO MMOJA WEKA JUUUUUUUU!!!

Mambo yoote ni IJUMAA hii pale SUN CIRO kwa viingilio hivyo vinavyojionesha hapo juu!!

Wednesday, June 2, 2010

HATIMAE THEA AAMUA KUOLEWA...........

Ni wasanii wachache sana wa kike katika tasnia ya filamu ambao wameingia kwenye swala la ndoa, Wengi waliobakia bado wapowapo sana na hata ukiwauliza swala la ndoa watakujibu hawafkirii kwa sasa..

Kwa upande wa Thea huu ndio wakati wake wa kuingia rasmi kwenye ndoa kwa sasa ambapo anatarajiwa kuolewa mwanzoni mwa mwezi wa kumi na jamaa anaefahamika kwa jina la MIKE SANGU ambae aliwahi kuwa katika sanaa ya maigizo miaka ya nyuma sana.

Kikao cha kwanza cha KITCHEN PARTY kitafanyika JUMAMOSI hii ya tarehe 5 JUNE 2010 maeneo ya Kinondoni pale OASIS PUB.

HONGERA SANA MAMAA na KILA LA HERI...

Tuesday, June 1, 2010

POLENI SANA!!

Kwa muda kama wa wiki nzima nilikuwa kimya na hakukuwa na kipya chochote ndani ya Blog yetu hii sababu kubwa ikiwa ni MALARIA kali iliyopelekea mpaka kulazwa hospitalini, na si kwenye blog tu bali hata kazini sikuweza kufika kwa kipindi chote hiko na hivyo kutosikika kwenye mambo yetu yale ya movie.. Nimepata message nyingi sana za lawama kwa upande wa blog sababu hawakuwa wanajua kinachoendelea..
Naomba nichukuee nafasi hii KUOMBA RADHI kwa hilo.. kwa wale wadau poleni sana.. Tuko pamoja
Asante.

USIKOSE CLOUDS TV LEO USIKU

PAUL JAMES na SHAFII DAUDA

Utamu wote uko hapa leo hii ukizingatia KOMBE LA DUNIA ndio liko njiani..

Umezoea kuwasikia lakini leo utawaona LIVE kabisa ndani ya CLOUDS TELEVISION wakikuchambulia mambo mbalimbali kuhusiana na SOKA kwenye kipindi chao "ROAD TO SOUTH AFRICA"

NI LEO HII ndani ya CLOUDS TV saa TATU NA NUSU usiku.. USIKOSE!!!!