Friday, February 26, 2010

THIS IS IT!!.. IS IT??


Steven Kanumba 'THIS IS IT'

Kuna FILAMU mpya inakuja kuhusiana na Kanumba inaitwa THIS IS IT, hatujui kama itakuwa na chochote kuhusiana na MICHAEL JACKSON ukizingatia kwamba kuna MOVIE ya Michael Jackson inayokwenda kwa jina hilo ambayo ilizinduliwa 28th October 2009.
Lakini kwenye Cover la Kanumba tumeona kuna vitu vingi sana ambavyo vinashabihiana na Michael Jackson(Alivyopenda kuvifanya) kama vile kitendo cha kupenda watoto na kanumba anaonekana akiwa na watoto, pia Uvaaji wa kofia ni kitu alichokipenda michael Jackson na Kanumba anaonekana akiwa amevaa Kofia inayofanania na alizokuwa akipenda kuvaa Michael.

Si kitu kibaya Kujaribu kuthubutu kitu kama hiko ila since hatujajua story yenyewe inahusu nini huenda pia akawa ameamua kwenda level nyingine kwa 'KUDANCE' kama Michael.Kuna wengi waliojaribu kucheza kama Michael Jackson lakini hawakuweza kumfikia The King of pop, mfano mzuri ni watu kama Jamie Fox ambae hakuweza, Usher Raymond who was good in Dancing lakini hakuwa Michael, mwingine alieonekana Kujitahidi kidogo kuliko wengine ni Chris Brown lakini bado Michael alibaki kuwa Michael.
Ukimuangalia Kanumba hapo juu SIZE yake ni kubwa kidogo compared to Michael Jackson who was not big. sasa hatujui kama ataweza kuwapiku walioshindwa ama la kama story yenyewe itahusiana na mambo ya Dancing.ila kama ni Cover tu na jina la kuuzia Filamu tunasubiri tuone huenda story ikawa tofauti.

Dancing Movies kwa hapa Tanzania ni kitu kigeni kidogo,ila kama Kanumba atakuwa amejaribu kufanya hivyo, we will be interesting to see.
Michael Jackson 'THIS IS IT"

Baadhi ya vipande vya THIS IS IT ya Michael Jackson



7 comments:

Anonymous said...

mara ya kwanza nacomment hapa,angetafuta jina lingine. This is it? hell no.
J

Anonymous said...

wivu tu jina zuri sana hilo hata kwa kuuzia hata kama filamu bado hatujaiona.

Christine said...

Tatizo letu Wabongo tunaangalia soko kuliko ubora wa filamu ndo mana hatufiki popote na filamu ukiiangalia mara moja hutamani hata kuirudia tena, angetafuta tu jina lingine kwani huku ku-copy and paste hakutatufikisha kokote. Hata mimi na support jina hili HELL NO

Anonymous said...

Tunaisubiri, lakini isiwe copy and paste we just change the language basi.


disminder.

Anonymous said...

Zamaradi inabidi uwe active kwenye blog yako kusudi upate followers wengi my dear,weka picha nyingi badala ya maelezo mengi.watu wengi wanapenda kuona picha kwanza then ndio wanasoma what you wrote.I LIKE YOU GIRL.

Anonymous said...

duu noma sasa kama this is it ya mtu mzima michael km ya kudance sawa sasa si itabidi kuimba je ataweza?,manake mambo ya kikristu pale me naona kazi ipo ila litakuwa jina tu anataka kuuza tu,ila wabongo no creativity bwana.

Anonymous said...

mambo zenu!
tatizo lako zamaradi unatoa mawazo yako badala ya kutoa habari watu wachangie tayari ulishamkosoa sasa watu wachangie nini ??? na jina sio kitu cha kushangaza inategemea na story