Friday, October 28, 2011

MOJA YA SCENE ZILIZOWAHI KUNIFURAHISHA ZA FILAMU...


Haimaanishi kwamba hiyo filamu ndio the best film hapana, ila ninachozungumzia ni kipande nilichokipenda ambacho kinapatikana kwenye filamu inayofahamika kwa jina la MTAANI KWETU..
Kizuri lazima kisifiwe na hata pale tunapoenda tofauti lazima tuongee pia lengo ni kusonga mbele zaidi na hakuna chuki binafsi..

Hiko ni kipande kinachomuonesha Richie kama mtu aliepoteza mtoto wake sasa anakwenda polisi kuripoti akiwa na jirani yake kufika huko kuna madhila yanayomkuta pamoja na kwamba amepotelewa mtoto wake...

Nikikiangalia hiki kipande mara nyingine kinanichekesha kutokana na Transformaton ya uso wa Richie ambae mwanzo aliingia na mbwembwe zote polisi huku akionekana mjuaji na mjanja mwingi lakini anapopewa kibano na anapobadilika hata uso wake unabadilika na anaonekana mdogoo tofauti na alivyokuwa mwanzo..

Kikubwa ni uhusika aliouvaa Richie na wote wengine, lakini kwa richie zaidi ni ule uhusika wa uso wake ulivyokuwa na ile transformation ya hatari iliyotokea kwenye uso wake..

Zaidi angalia hapo juu...

MJUE MSANII SHAMSA FORD...

Wednesday, October 26, 2011

THE LOST ADAM - moja kati ya filamu nilizozipenda kwa mwaka huu...



Nimeangalia filamu nyingi sana kwa mwaka huu na hiyo ni kutokana na kazi yangu pia.. Kiukweli kuna improvements nyingi sana kwenye filamu zetu kwasasa lakini mara nyingi kitu ambacho huwa kinatuangusha ni STORY za filamu zetu.. nyingi ziko too shallow, na haya mambo ya part one na two ndio kabisa yanazidisha u-shallow kwenye filamu

Lakini pamoja na kwamba story nyingi ziko Shallow, bado kuna watu ambao wanaendelea kufanya vizuri kwenye filamu, ambapo hata kama story ni ya kawaida utakutaSCRIPT yake imesimama na hata DIRECTOR anakuwa ameitendea haki kiasi kwamba unaangalia filamu na unaona kabisa kwamba hii filamu imedirectiwa..

Moja kati ya filamu nilizoziona na zikanifurahisha kwa mwaka huu.. ni filamu ambayo imedirectiwa na Mtitu Game ambayo inaitwa THE LOST ADAM..

Kikubwa ni Uchezaji wa baadhi ya watu humo ndani.. ni kwamba wamefanya vizuri sana nikianzia na ROSE NDAUKA ambae amevaa uhusika vilivyo kabisa, JACOB STEVEN(JB) pia amefanya vizuri sana na naweza kusema huyu ni mtu ambae kwa movies zake nilizowahi kuangalia naweza kusema Hajawahi kuniangusha.. pia kuna Patcho Mwamba, Hemed Suleiman na wengine wengi ambao kila mtu amekamua kwa nafasi yake..

Kikubwa nampongeza sana Director wa hii filamu kwa kazi aliyoifanya kwani ukiangalia filamu yenyewe unaona kabisa kwamba imekuwa directed na mtu ambae yuko serious na anaijali kazi yake, ila zaidi angalia hiko kipande hapo juu ambacho ni MOJA kati ya SCENES nilizozipenda sana kwenye hii Filamu..

Tuesday, October 25, 2011

USIKOSE TAKE ONE LEO USIKU on CLOUDS TV


Usikose TAKE ONE siku ya LEO saa TATU KAMILI USIKU on CLOUDS TV na Zamaradi Mketema!!

Thursday, October 20, 2011

DAD and SON.. soo lovely!!


Allen Mushi na mtoto wake jayden!

PICHA YA LEO.. warembo wa bongo movie!!


Wema kajala na lulu!!

KWA KUMSIKILIZA LULU AKIONGELEA MWENYEWE KUHUSIANA NA JUSTIN BIEBER.. BONYEZA HAPO CHINI!!!

LULU na JUSTIN BIEBER by nelly@g5click.com

LULU na JUSTIN BIEBER by nelly@g5click.com
Hiyo ni Interview niliyofanya nae kwenye redio ambapo amejielezea mwenyewe kiurefu zaidi kwamba, NI kweli?? na kama kweli ni kimapenzi ama kishabiki?? na pia Bieber akitaka mapenzi klwake itakuwaje??
Kwa majibu yote msikilize LULU hapo juu!!!

Wednesday, October 19, 2011

HEMED na MLELA kuja kivingine..

tegemea kuwaona katika filamu mpya kabisa itakayotoka hivi karibuni ambapo wameigiza character tofauti kabisa wakiwa mererani kwenye machimbo
ukiangalia juu juu hapo unaweza usiwatambue harakaharaka kwa jinsi walivyojiweka na muonekano wao ulivyo
hapa akipewa dozi na wamasai wa mererani
coming soon!!

HII NI KWELI..!!?? lol





























Hebu angalia hizo picha hapo kwa umakini sana halafu uniambie kuna ukweli wowote katika maana zilizotolewa kwenye hizo aina za ulalaji wa mtu na mpenzi wake!??

Niambie WEWE na YEYE mnahusika kwenye ipi zaidi kati ya hizo hapo juu!!?? na ukiangalia aina yenu ya ulalaji inaendana na jinsi mahusiano yenu yalivyo!!???

LET'S SHARE

Tuesday, October 18, 2011

USIKOSE TAKE ONE LEO na kila JUMANNE kupitia CLOUDS TV saa TATU KAMILI USIKU!!

MLOPELO AILALAMIKIA CLOUDS KWA KUTOPIGA WIMBO WAKE


Msanii wa siku nyingi wa maigizo MLOPELO ambae alikuwa akiigiza kama jini mara nyingi kwa enzi hizo kupitia kaole ameibuka na kuilalamikia CLOUDS kwa kutopiga wimbo wake ambao kwa mujibu wa yeye anasema uko kwenye mahadhi ya R n B..
Kwa kuusikiliza wimbo huo na malalamiko yake bonyeza hapo juu ili uweze kuuusikiliza vizuri wimbo huo na kusema yaliyomo yamo!!!

Monday, October 17, 2011

LULU ANATARAJIA KWENDA EUROPE KUMTAFUTA JUSTIN BIEBER.. ANASEMA ATACHANGISHA HATA KADI KWASABABU HIYO...

Msanii Star wa filamu ambae alianza kuigiza akiwa na umri mdogo ameamua kufunguka na kuweka wazi kwamba ana mpango wa kwenda EUROPE kwa sababu moja tu ya kumtafuta JUSTIN BIEBER....

Nilipomuuliza sababu ya kumtafuta kama ni ya kishabiki ama ya kimapenzi alijibu kwamba ni kishabiki lakini lolote pia linaweza kutokea,Lakini hapohapo nikataka kujua kama amesahafanya juhudi zozote za kuwasiliana nae akasema kwasasa bado hapana ila anachotaka kufanya ni hiko kumuendea hukohuko kumsaka..

Kuhusiana na NAULI nilipotaka kujua amejipangaje LULU akasema atachangisha kadi kwasababu anaamini kitendo anachotaka kukifanya ni cha kimaendeleo na ni UJASIRI mkubwa kwasababu amejitosa kwenda kumtafuta mtu ambae hapatikani kirahisi hivyo ni USHUJAA..

kabla sijamaliza interview nae nilimuuliza lulu ikitokea bahati akakutana nae na mara itokee JUSTIN BIEBER nae amevutiwa na yeye KIMAPENZI, je atakuwa Tayari!!??? alichonijibu ni kwamba YANI BILA KUULIZA YUKO TAYARI KABISA na hilo sio swali la kuuliza kwani bila wasiwasi atafanya hivyo..

Soon nitakuletea CLIP ya sauti ya interview ambayo nilifanya nae!!

Monday, October 10, 2011

HALI YA KIAFYA YA MZEE KIPARA SI YA KURIDHISHA SANA...

Nilipata nafasi ya kumtembelea kama mara mbili hivi kwenye wiki hizo zilizopita na kiukweli kabisa ukiangalia hali yake kiafya kwasasa naweza kusema ni kama hairidhishi.. Hii ilikuwa mara ya kwanza nilivyokwenda kumuona ambapo alikuwa akiweza hata kuinuka na kutembea kidogo
Lakini nilivyorudi mara ya pili hali ilikuwa kama tete hivi sababu hata uwezo wa kutembea mwenyewe vizuri kwasasa hana, akitaka kusimama lazima ashikilie ukuta na hata akitaka kutembea anakuwa anatambalia ukuta ambao nao naweza kusema si kwamba unamsaidia, haumsaidii chochote sababu hujikuta anaanguka pia..
Hivyo muda mwingi kwasasa huutumia kulala tu, na amekuwa hajiwezi kwa chochote kwasasa, na hata kujisaidia pia saa nyingine hujikuta anamalizia sehemu aliyokuwa saabu nguvu za kuinuka hana...
Kwasasa mzee Kipara anakaa Kigogo kwenye nyumba ya Kaole chini ya Uangalizi wa kaole ambapo kuna kijana waliemuweka ambae ndio anamsaidia bega kwa bega katika kumuuguza na kumtunza, hivyo kwa mtu yoyote ambae atatamani kwenda kumuona anaweza akafika kigogo pale na kwenda kumuona...
Kikubwa tumuombee tu aweze kurudi katika hali yake ya zamani, ambapo nakumbuka zamani ulikuwa ukienda kumtembelea alikuwa akipata hadi nguvu za kukusindikiza tofauti na sasa ambapo hata kutoka nje ya chumba chake tu ni tabu na kikubwa anacholalamikia ni miguu pamoja na kwamba kuna maradhi mengine yanayomsumbua pia...

KAJALA - MTOTO WANGU NDIO KILA KITU KWANGU


Hii ilikuwa kupitia kipindi cha TAKE ONE ya Clouds TV ambapo Kajala aliweza kufunguka vitu vingi sana kuhusiana na maisha yake ikiwemo mahusiano yake yaliyopita na P.funk jinsi walivyokuwa wakiishi, siku ambayo hataisahau ambapo aliwahi kupelekwa segerea,kitu kilichosababisha na vitu vingi kuhusiana na maisha yake..

Kwa hayo na mengine mengi bonyeza hapo juu (kwenye video yake) ili uweze kumsikia na kumuona mwenyewe akiongelea kuhusiana na maisha yake!!!!

Friday, October 7, 2011

JINSI WEMA SEPETU ALIVYOVALISHWA PETE NA DIAMOND..


Kwa wale ambao hawakufanikiwa kufika kwenye tukio, ama waliomiss kipindi cha TAKE ONE ya CLOUDS TV, hivyo ndivyo hali ilivyokuwa ambapo siku ya tarehe 2 october kwenye sherehe ya kuzaliwa ya Diamond, aliamua kumfanyia suprise mpenzi wake WEMA kwa kumvalisha pete mbele ya hadhara ya watu..
Maneno matupu hayatoshi... Hebu enjoy the video hapo juu!!!

SIJUI NIELEZEE VIPI NIELEWEKE LAKINI JUA TU NAUPENDA HUU WIMBO KULIKO MAELEZO YENYEWE...



Ukiniuliza sababu naweza nisiwe na ya maana sana ya kukupa lakini kwakweli NAUPENDA huu wimbo kuliko kawaida, na nikiwa nausikiliza huwa sipendi kabisa bugdha na ni moja kati ya nyimbo ambazo nikizisikia zinaniingia ile kabisa moyoni ( i feel this song for real yani),Kwa kifupi naweza nikasema ujio mpya wa Sumalee UMETISHA!!!!

Nikianzia na mistari jinsi ilivyopangwa kuna kama kaubunifu fulani hivi kametumika kwenye vina, mdundo wake kama wa ki-kwaitokwaito hivi, na hata idea ya wimbo kwa ujumla..Kiufupi huu wimbo Unanimaliza.. Big Up kwa hilo Suma!!

Tukirudi kwenye Video ndio kabisa yani.. nimependa jinsi wanavyocheza humo ndani, its really nice na kingine hata sumalee mwenyewe mwanzo kama haonekani hivi, anakuja kuonekana mwishoni mwishoni mwa wimbo!!! Sidhani kama masikioni mwangu utachuja leo ama kesho.. na mara nyingi huu wimbo ukipigwa nashindwa kuvumulia, ntainuka tu kama nna nafasi hiyo, na hata kama sina nafasi basi hata ntashtuka tu bila kutegemea!!!

NAMSHUKURU SANA SUMALEE kwa kuniongezea furaha kwenye siku yangu ya kuzaliwa kwa kunipa ka-suprise kadogo ambako kana maana kubwa sana kwangu, nafikiri alijua ama alinisikia nikisema kwamba huu wimbo naupenda sana, nilipigwa na butwaa siku ya birthday yangu baada ya Babu tale kunipigia simu na kuniambia kuna mtu ana zawadi yangu nimsikilize ghafla akampatia simu mtu na nikashikwa na butwaa nilivyosikia sauti ikiniimbia HAKUNAGA ambapo sauti hiyo ilikuwa ya sumalee mwenyewe.. I felt soooooo GOOD aisee and i really really appreciate kwa hilo suma...

KIUKWELI HATA KAMA KUNA MTU ANAUPENDA HUU WIMBO SIDHANI KAMA ATAKUWA KANIZIDI MIMI...

I LOVE the SONG!!!

PICHA TU ZA KUMALIZIA...


keki yangu ya pili on my birthday!!!


picha tu za kumalizia...

UNAMKUMBUKA MBONI MASIMBA KWENYE HII VIDEO!!???


Wimbo unaitwa ZUWENA..

Moja kati ya nyimbo ambazo ziliwahi kufanya vizuri na kutamba sana hapa Tanzania kwa kipindi hiko kutoka kwa Mr. Paul ambayo ilikuwa ni katika zile zilizowahi kufanyiwa Copy kutoka kwa wanamuziki wa zamani...

Hivi unafahamu msichana alietumika kupamba video hiyo na kuifanya ivutie zaidi ambapo ndio aliigiza kama Zuwena kwenye hii Video ni MBONI MASIMBA a.k.a Kim K!!???
kama ulikuwa hufahamu hebu icheki hiyo video vizuri.....

Tuesday, October 4, 2011

ASANTE SANA SHAMSA for the CAKE!!!

Nimemzoea kwa jina la SHAMSA ingawa wengi wanaomfahamu kwasasa humuita SHAMSA FORD ambalo ndio jina lililomtambulisha kwenye fani,

Ukiangalia nature ya kazi zetu ambapo yeye ni muigizaji wa filamu na mimi ni mtangazaji wa kipindi kinachohusiana na Filamu unaweza ukahisi labda tumekutana kupitia kazi zetu, lakini sivyo ilivyo..

Mimi ni shamsa hatujajuana jana wala juzi, na wala hatukukutania ukubwani ila ni mtu ambae ukiuliza rafiki wa zama ni yupi basi utatajiwa Shamsa, ni rafiki yangu wa muda mrefu SANA ambae tumepitia mengi pamoja, shida, mitihani, raha na mambo yote tunakuwa wote
Ni mmoja kati ya watu muhimu sana kwenye maisha yangu, ni mtu ambae ananifahamu mimi vizuri kuliko chochote kitabia na kilakitu (mbaya na nzuri..lol) na hata mimi pia namfahamu yeye ile yenyewe yenyewe kabisa, so kiufupi tunajuana vizuri na ni marafiki wa muda mrefu sana ambao tumesaidiana sana kwenye raha na shida.
Leo mapema asubuhi hata kabla sijaamka ametoka nyumbani kwake mpaka kwangu lengo likiwa ni moja tu kunisuprise pamoja na KEKI hiyo unayoiona hapo.. Am really happy kiukweli na nathamini sana alichonifanyia, it means alot to ME!!!

Kwa leo sina mengi sana ya kuongea ila zaidi ni kukushukuru kwa kuweza kutambua siku yangu hii muhimu na kufanya kitu cha kuweza kunipa na kuongeza furaha katika siku yangu... Thats what friends are for!!!..


Nakupenda sana... Together Forever!!!

Monday, October 3, 2011

I CANT WAIT FOR MY BIRTHDAY KESHO.. SHUKRANI KWA MAMA YANGU PAMOJA NA WOTE WALIO KWENYE MAISHA YANGU.

Katika tarehe ambazo nazipenda basi nafikiri tarehe 4 ya mwezi wa KUMI itakuwa inaongoza sababu ndio siku niliyozaliwa..
Nakumbuka kwa mwaka niliozaliwa ilikuwa ni Ijumaa lakini kwa mwaka huu tarehe yangu ya kuzaliwa imeangukia Jumanne ambayo ni KESHO....
Always naipenda sana hii siku na naithamini sana na hata kama mtu atanikera kwenye hii siku huwa sipendi kumpa nafasi ya kuharibu siku yangu
I have so many people to THANK lakini mkubwa kuliko wote ni MUNGU ambae bila yeye hakuna mimi na naamini mambo yote yanayonitokea ni matokeo yako WEWE ya-ALLAH, nakushukuru kwa yote na kubwa zaidi kwa kunipatia wazazi ambao umenipatia.

Nikizungumzia wazazi nazungumzia BABA na MAMA... Napenda sana kuchukua nafasi hii kutoa heshima kubwa sana kwa my lovely DAD ambae tayari ameshatangulia mbele ya haki, naamini asilimia kubwa ya Zamaradi anaeonekana leo ni matokeo ya malezi yako wewe, umenilea kwa mapenzi makubwa sana ambayo yalinijenga kwenye mambo mengi sana na kubwa kuliko yote ikiwa ni kujiamini sababu always ulikuwa ukiniambia AM THE BEST na nimekuwa nikiamini hivyo mpaka leo hii. Hivyo kujiamini ulikonijengea kunanisaidia kwenye mambo mengi sana katika maisha yangu mpaka leo hii. Upumzike kwa amani!!!

Nikirudi kwa upande wa MAMA nafikiri inajulikana kwamba hakuna kama MAMA duniani, mama ndio kila kitu na napenda kuchukua nafasi hii kumshukuru kwa mapenzi ya DHATI na UKWELI alionionesha tangu utotoni na ambayo anaendelea kunionesha mpaka leo.. mapenzi yako hayalingani na mtu yoyote katika dunia hii, wewe ni mtu ambae hata wote wanitenge wewe utakuwa upande wangu, ni aina ya mtu ambae maumivu yangu ni maumivu yako, ni mtu ambae unafurahia kwa dhati kabisa mafanikio yangu na pia ni mtu ambae Unaumia kiukweli na kuanguka kwangu...


Hakuna zaidi yako mama


LOVE YOU MAMA, VERY PROUD OF YOU!!!!!
Mama kiufupi siwezi na wala hakuna neno ambalo litaweza kuexpress mapenzi yako lakini kubwa tu jua NAKUPENDA, NAKUJALI na NAKUTHAMINI kuliko chochote, na kila ninalolifanya kwenye maisha yangu ni kwa sasabu yako.. siwezi kulipa hata robo ya ulichonifanyia sababu mapenzi yako hayafananishwi na chochote, unachotakiwa kujua ni kwamba NAKUPENDA kuliko chochote kile.. wewe ndio kila kitu kwenye maisha yangu, wewe ndio mboni yangu na wewe ndie mzazi pekee uliebakia kwangu, HAKUNA KAMA WEWE MAMA!!

Kuna wengi sana wa kuwashukuru ambao ni ngumu kuwataja wote lakini siwezi kumuacha mdogo wangu wa Pekee ambae huyu ni kilakitu kwangu.. naweza kusema ni kama zawadi aliyoniletea mama baada ya kuishi kwa muda mrefu kidogo bila mdogo wangu .. UMMY nakupenda sana na unalijua hilo, umekuwa ukinisupport kwenye vitu vingi sana katika maisha yangu pamoja na kwamba you are young to me lakini umejitahidi kuwa mshauri mzuri pale ninapohitaji ushauri kutoka kwako.. lol!! Love u soo much ma!! I am your another MAMA.

Watu ni wengi mno waliofanikisha zama kuwa zama, bila kusahau rafiki zangu wote ambao tumeweza kusaidiana kwenye mambo mengi sana shida na raha nyingi tuko wote, na hapa nazungumzia watu wote ambao wamewahi kuwa watu wazuri kwangu kwa kipindi tofautitofauti.. SHAMSA FORD, IRENE, HILDA, nawapenda sana sana wote na nataka mjue kwamba nathamini hata kile kidogo ambacho mliwahi kufanya kwangu haijalishi kwamba mko karibu ama mbali na mimi kwasasa.
Katika vitu ambavyo nimebarikiwa na namshukuru MUNGU ni kuwa na marafiki wengi, I have so many friends kiasi ni ngumu kutaja wote lakini hata kama sijakutaja jua nakupenda na kukuthamini, Hifla, Salome, Edith, husna bila kumsahau Ada(mama malcom) ambae amekuwa akinilea kwenye vitu vingi sana kama mtoto wake (nizoee mama ndivyo nilivyo) lol..

Ukiachana na hao pia napenda kuwashukuru wafanyakazi wenzangu pia ambao tumeweza kuishi vizuri kwa kipindi chote hiki, wengi nikiwa nimewakuta na wakanipokea vizuri mpaka leo hii,tumekutana kwenye mazingira ya kazi lakini tumejikuta tunashirikiana kwenye mambo mengi sana na kuunda urafiki kwa baadhi yao, ni ngumu kutaja wote lakini jua tu nawapenda sana pia.. Mully B, Dina Marios, Da Geah habib (VIP) hahaaa unajua huwa tunasumbuana wapi, Kibonde, Kayanda, venture, dee, Junior, Raymond Charles, P.diddy, da asma, Da Regina,Simalenga, Nugaz, dozen, Mwabulambo, bonge,barbara hassan, Babu tale (jirani), Suka, Jimmy jam, Soudy Brown (naomba flash. lol) Gerald hando ambae amekuwa ni mshauri wangu kwenye mambo mengi ya kikazi, Reuben ndege, brother Sebastian na wafanyakazi wenzangu wooote.. Dah ni ngumu sana kutaja wote maana ni wengi mno lakini nawathamini woote!!!

Pamoja na MA-FANS wangu woote ninaowafahamu na nisiowafahamu wote wanaonissuport nawashukuru sana!!

Bila kumsahau Boss wangu Ruge Mutahaba ambae ameweza kunionesha mwanga kwenye mambo mengi sana pamoja na maboss zangu WOOTE!!
SHUKRANI ZA DHATI na MUNGU AWABARIKI WOTE!!!

UNAMKUMBUKA HUYU!!!????



Anaitwa MLOPELO, kwa wale ambao ni wafUatiliaji wa maigizo ya kaole kipindi hiko hatakuwa mgeni kwenu, alikuwa akiigiza kama mchawimchawi hivi akishirikiana na bi mwenda enzi hizo, ila kwasasa ni kama amesimamisha shughuli za sanaa kwa muda kutokana na maradhi yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda wa miaka miwili..

Mlopelo kwasasa anakaa kwao maeneo ya TEMEKE akiwa kwa wazazi wake, hajaoa na wala hana mtoto..

Kwa kumuangalia kutokana na umbo lake unaweza ukahisi labda ni mdogo kiumri lakini huo ni udogo wa umbo tu ila kiumri amejaaliwa kula chumvi kidogo kwani kwasasa ana UMRI wa miaka Thelathini na tisa (39).


Mlopelo mbali na sanaa ya uigizaji pia ana kipaji kingine cha kuimba ambacho alifanikiwa kutuonesha ingawa analalamika kwamba redio hazipigi nyimbo yake.

Muda si mrefu nitakuletea kipande cha interview niliyofanya nae ili uweze kujua kwasasa yuko wapi, anafanya nini, pia kipaji chake cha uimbaji nakadhalika...

NAOMBA RADHI KWA KUWA KIMYA KWA MUDA WOTE HUO

Nimekuwa kimya kwa kipindi cha takriban mwezi mmoja sasa, kuna wengi wametuma comments negatives and positives kulalamikia hali ya ukimya wangu.. lakini kiukweli kabisa kwa wote waliotuma comments ziwe mbaya ama nzuri nathamini sana kwakuwa mnanithamini pia na ndiomana mnapoingia na kukuta hamna kitu,kidogo mnakuwa mnakwazika na kuongea vile ambavyo mnaongea..

Siwezi kutoa sababu ya ukimya wangu sababu ni nje kidogo ya uwezo lakini sababu haikuwa ni kukosa habari ama vitu vya ku-update sababu katika maisha ninayoishi kila siku nimezungukwa na habari kuanzia kwa wenzangu walionizunguka mpaka kwenye vipindi ninavyofanya on TV and radio hivyo sio mtu wa kukosa cha kuweka humu.. ila ninachoweza kusema ni mambo tu yaliingiliana na kauzembe kidogo kutokana na kutingwa na vitu vingine naomba nikiri hilo.. hivyo kutokana na sababu hiyo ambayo wengi wenu hamtanielewa sina budi kuchukua nafasi hii KUOMBA RADHI KWA WOTE ambao hawakupendezwa na hili..

Nawapenda WOTE mnaonipenda na kunichukia sababu naamini wote mna sababu za kufanya hivyo na hata kwa wale wanaonichukia bila sababu pia nawapenda sana sababu kuna sababu ambayo wao wenyewe wanaweza wasiijue ama wanaijua lakini wanashindwa kukubali kwamba ndio hiyo hivyo salute kwenu wote sababu mnazidi kunipa changamoto kwenye maisha yangu...

Naamini kila anaeingia humu iwe kwa nia mbaya ama nzuri ananikubali na ni mtu wangu na ndiomana tunaendelea kuwa pamoja!!!!

I AM WHO I AM.. what you see is what you get!!!

LOVE YOU ALL....