Wednesday, April 21, 2010

MZEE YUSUPH AANGUKA GHAFLA LEO...

Hapa ilikuwa ni harakati za kumuingiza kwenye gari kwa ajili ya kumuwahisha hospitali.

Ilikuwa mishale fulani ya sasa sita, mwanamuziki wa kundi la taarab la JAHAZI alipokuja clouds FM leo kwa shughuli zake binafsi lakini ghafla tu wakati anaingia ndani mguu ukashtuka ukawa umekaza na unashindwa kunyooka kabisa, akaomba kiti akae lakini ghafla nyonga nayo ikakaza ikabidi atandikiwe chini ajinyooshe huku utaratibu wa kumpeleka hospitali ukiwa unashughulikiwa..

mara akakimbizwa Hospital ambako yuko mpaka sasa na ripoti ya daktari inasema ni mshipa umekaza kitu ambacho kinaweza kutokea saa yoyote hivyo amechomwa sindano na baada ya nusu saa huenda akarudi kwenye hali yake ya kawaida..
Get well soon!!

1 comment:

sophy said...

asante zam dah tunamuombea apone maana sisi wengine ni wapenzi wake sana