Tuesday, April 6, 2010

BURIANI BABA

PASAKA YA MWAKA HUU NIMEISHEREHEKEA KATIKA HALI YA MAJONZI MAZITO KUFUATIA KIFO CHA BABA KILICHOTOKEA JUMAPILI NA MAZISHI KUFANYIKA JUMATATU JANA KWENYE MAKABURI YA KISUTU JIJINI DAR. PICHANI JENEZA LENYE MWILI WA BABA LIKITOLEWA NYUMBANI NA KUANZA SAFARI YAKE YA MWISHO KUELEKEA MSIKITI WA MTAMBANI NA KISHA MAKABURINI. NALIA NASIKITIKA KUBAKI MKIWA. HATA HIVYO KAZI YA MOLA HAINA MAKOSA. MOLA IWEKE ROHO YA MAREHEMU BABA MAHALA PEMA PEPONI - AMINA

28 comments:

Anonymous said...

POLE SANA SIS ZAMARADI
MUNGU AWAPE MOYO WA SUBRA KWA KUONDOKEWA NA MZEE
M MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALA PEMA PEPONI AMIN,POLENI SANA
From G Recordz Crew

sechelela said...

pole sana my dear

de'victorious said...

pole zama kazi y amungu haina makosa nipo nawe ktk kipindi hiki kigumu...

samira said...

inalillah waina illaih rajuun...pole sana ma dia

Anonymous said...

pole sana..im sure he will be missed.

Ngoi said...

Ya mamaangu majonzi yetu sote.Maana bora ya nyie mliobahatika hata kumzika kuliko sie tuliokuwa mbali huku ambao tumeishia kuzika kwa cm tuu. Pepo ndo kitu sie sote tunamuombea. Ila ndo hivyo kazi ya Mungu haina makosa. Bwana katoa, na bwana kachukua.

Anonymous said...

pole sana zamaradi
mungu atakupa nguvu tu!
MAMA TRACE

Christine said...

Pole Zamaradi, bwana alitoa na bwana ametwaa jina la bwana limebarikiwe.

Anonymous said...

Pole sana Zamaradi mpenzi hata mi nilifiwa na baba najua ni pigo kubwa na nilichukua muda kulizoea. your fan ibrahim.

Sarp said...

Pole saa Zama..Munu ailaze roho yake mahala pema peponi.

Anonymous said...

inna lillahi wa inna illahi rajiun... pole kwa familia yako yote.

Anonymous said...

pole sana zamaradi,uwe na subira katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na baba yetu mpendwa.sisi tulimpenda lkn mungu amempenda zaidi.

ALIVYO TUTAKUA,TULIVYO ALIKUA.
inna lilahhi waina illai rajiuun.
mdau saudi.

MloMmoja said...

Mwenyezi amrehemu dad yako na awape nguvu na imani ktk kipindi iki kigumu cha maombolezo,.Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un

Baba claire a.k.a dickdada said...

pole sana mwenyezi mungu ailaze roho yake mahali pema na pemoni

Unknown said...

RIP BABA

Anonymous said...

pole dada kazi ya mungu,muenzi baba kwa kufanya yale mazuri aliyokua akikusisitizia.

Majoy said...

Pole sana Zamaradi kama ulivyosema kazi ya mola haina makosa.

Majoy said...

Pole sana Zamaradi kama ulivyosema kazi ya mola haina makosa.

bestinox said...

Inallillah Waina Illah Rajiun..Pole dada yangu ni kazi ya Mungu haina makosa..kubwa ni kuwaombea dua wote waliotangulia Mungu awaweke mahali pema Peponi..Pamoja katika Maombelezo.

Anonymous said...

hey,pole zama mungu alimpenda zaidi ni kazi ya mungu haina makosa please stay strong kwa kipindi hiki kigumu kwako dont cry dats life baby let it go n let god deal with it,life goes on may god rest his soul in peace...Amen

Anonymous said...

Pole sana Zamaradi, Its so painful kumpoteza mzazi..
Mungu akupe faraja wewe na mama

Anonymous said...

Pole sana Zamaradi.

Mdau Finland

Anonymous said...

pole zamaradi ndugu kwa kufiwa katika dunia hiii hakun kiumbe ambacho hakita onja mauti,cc sote tuko ktk safari hiyooo ucuzunike sana kwani huko aliko yuko kwenye pumziko la milele mungu ailaze roho ya marehemu wote amina

Anonymous said...

Pole sana! Mungu akupe nguvu sasa na hata siku zote. RIP Mzee wetu!

Anonymous said...

Sisi sote ni wake MOLA nasi kwake tutarejea! Kwani yeye ametangulia nasi tutafatia. Mungu amlaze pahala pema peponi. Poleni sana!

JACKIE said...

POLE SANA ZAMARADI,MUNGU AKUTIE NGUVU WEWE NA FAMILIA YAKO.

Zamaradi said...

ASANTENI SASA SANA kwa maneno yenu ya faraja kwangu.. nashkuru sana na MUNGU awabariki wote
Tuko pamoja daima!!

Hans Megrah said...

INNA LILLAHI WAINNA ILAYHI RAJIUN.Pole sana bidada....Ila napatwa na wasi wasi pale unapolalamika kwamba Pasaka hukuisherehekea....Presumably, you are a convinced muslim, so I dont think you should support Pasaka...THINK ABOUT EID ZOTE MBILI AS THESE ARE SPECIAL FOR TRUE MUSLIMS LIKE YOU...However, Mungu akupe nguvu inshaallah.Hans Megrah..megrah@lycos.com