Friday, March 26, 2010

HIZI MAKE-UP ZETU KWENYE FILAMU NI SAWA KWELI??

Ukizungumzia Make-Ups watu wengi akili huenda moja kwa moja kwenye kupendeza, But when you talk about Make-up in film ni kitu tofauti kabisa.

Katika filamu huwa kunakuwa na uhusika tofautitofauti, watu huweza kucheza kama Mke wa mtu, Sugar mummy, changudoa, House girl, chizi, Jini, Mchawi n.k.

Na kama unavyojua kwamba Filamu ni Kuchukua maisha halisi na kuyaweka katika maigizo hivyo ni muhimu kumfanya mtu anaecheza sehemu fulani afananie na sehemu anayocheza ili aweze kuleta UHALISIA kwa maana ya kuvaa uhusika kamili si wa maneno tu bali hata KIMUONEKANO, kama ni Chizi inabidi aonekane chizi kweli,kama ni Changudoa muonekano wake inabidi uwe hivyo kulingana na sehemu anayocheza na SI KWA KUPENDEZA peke yake kama ambavyo wengi tunafikiria.

Hivyo maana halisi ya Make-ups katika Filamu ni kitu chochote ama ile hali ya kumbadilisha mtu ili aweze kuwa na muonekano na A-fit kwenye uhusika anaotakiwa kuucheza (kwenye sehemu husika) inaweza ikawa wa kupendeza ama kuchukiza. Let say mfano mtu anaweza akacheza kama MZIMU ama JINI anaweza akapakwa masizi, kwenye Filamu hata kama mtu amepakwa MASIZI ili atishe, hiyo kwenye filamu hatutaita masizi bali ni MAKE-UP.

So that’s HOW make-up inafanya kazi kwenye Filamu.

Lakini tukirudi kwenye filamu zetu za hapa nyumbani, maranyingi ma-MAKE-UP artist wetu wanafeli kwenye hili na sielewi tatizo linakuwa wapi, mtu anaweza akacheza yuko nyumbani tu kawaida AMETOKA KUAMKA lakini ATAREMBWA kupitiliza kiasi kwamba hata ule uhalisia huupati. Ama yuko kijijini hajawahi kufika hata mjini na maisha yake ni ya hali ya chini kabisa lakini kawekwa DAWA ama WAVE, haonekani kabisa kama ni wa kijijini kiasi kwamba anapoteza lengo zima la sehemu husika.

Kwa wewe mdau wa filamu uliefanikiwa kuangalia FILAMU kadhaa za hapa nyumbani hivi hizi make-up zetu ni sawa kweli?? zinaendana na mazingira halisi??

MATUMIZI YA MAKE-UP ZETU YANAENDANA NA MAANA HALISI?? AMA TUNACHOJALI NI MAUZO (KUPENDEZA) TU BILA KUANGALIA SEHEMU HUSIKA ANAYOCHEZA MTU?

Zamaradi Mketema.

3 comments:

Anonymous said...

Nilichangia GP watu wakanipaka sana tu. vipi hata mfanyakazi wa ndani anavutia kama boss wake.
hali halisi ya maisha yetu ni wachache sana wanaoishi mazingira hayo.


KIBATA
MDAU S.A

ANTI.BONGO MOVIE said...

unajua nini zamaradi Bongo tasnia ya filamu watu wanakurupuka sana ndo mana mpaka leo hakuna maendeleo ktk tasnia hii, watu wanauza sana sura yani unakuta mtu anajiremba mpaka anapitiliza afu ukiangalia scene anayocheza ni house gal au mfanyakazi wa kawaida. tatizo hili ni kwa wasanii wakubwa ambao ndo wamezidi. bongo tuna safari ndefu kama wanataka movie za bongo ziweke au kugombea tunzo nje ya tanzania waty wasome kwanza wasijidangaje kuwa kazaliwa na kipaji hiyo sio tija, bongo hakuna movie bali ni MAIGIZO tu.
Mdau. ANTI-BONGO MOVIE

Anonymous said...

Hii ni mar yangu ya kwanza kuchangia ktk hii blog! Ila hii mada kusema kweli imenigusa kama alivyosema mdau ANTI.BONGO hakuna "MOVIE STARS BONGO" Kwa sasa kwani wapo ambao wanataka kupata pesa za haraka! Najua kuwa hatujafikia level ya nchi za Western lakini watu wengi sasa wanauza sura. Haiwezekani with a week or two mtu anatoa movies 2 or more! Na pia the way wanavyokremisha maneno basi wanaonyesha kabisa "acting" and not real. wanatakiwa wawe wanaonyesha uhalisia wa maisha ya mtanzania. Na sio kuigiza kuwa wana uwezo wanaishi kifahari n.k!
Na sijui nani kawaambia kuwa kuongea kwa kufoka ndo kuigiza..yaani wanawaigiza NIGERIANS; hawajui kuwa wao nikutokana na lugha zao..
Tuache ushamba na tuanze kufanya mambo yetu na sio kuiga vitu ambavyo havitufikishi popote.
Mdau, US