Wednesday, July 13, 2011

PICHA MSETO... HAPA NA PALE



HAPO nikiwa na Barbara Hassan wa Power breakfast ya CLOUDS FM, hizi zilikuwa ni shamrashamra za Fiesta katika jiji la Mwanza ambapo tulikuwa tukizunguka mitaa tofautitofauti. Madereva walikuwa makini sana kusikiliza kinachoongelewa ili waweze kujibu maswali maana kilichokuwa kinaendelea ni Ugawaji wa mafuta ya BURE kabisa kutoka katika moja ya makampuni ambayo ni wadhamini wa Fiesta pia kwenye swala la usafiri wa ardhini GAPCO.
Hapo T-shirt ndio zilikuwa mpango.. mtu anaweza hata akakuvamia ili tu apate T-shirt za Fiesta.. watu wana mapenzi na fiesta mpaka basi aisee...
Nikiwa nafanya LIVE katika jiji la MWANZA kwa kushirikiana na Adam mchomvu ambae tulikuwa nae huko pia!!! Adam Mchomvu nae ndie huyo katika Live ambayo tulikuwa tukishirikiana..
Sijui nilikuwa naambiwa nini, hata sikumbuki lakini itakuwa kuna jambo nilikuwa nakumbushwa na Barbara Hassan. Hii ilikuwa ni LIVE kutoka Uwanjani.. Zamaradi, Adam pamoja na Reuben Ndege (Ncha kali)

1 comment:

Anonymous said...

Wakati mwingine km wakurupuka na mavazi yako usivae tu bora kuvaa. we unajua kbs unaenda kuwafanyia watu maswali kitaa eti unavaa heels na kimini ivi waijua vizuri kazi yako weye??????? tizama babra sio km hajui kuvaa la hasha kavaa kutokana na tukio yupo KIKAZI ZAIDI. Punguza shauzi mama