Wednesday, February 23, 2011

NIMEJIBU MASWALI YENU KAMA MLIVYONIULIZA.. KUHUSU MIMI!!


Mambo, vipi una mchumba au boyfriend? Kama unaye anaitwa nani?
ANS:
Sina mchumba ila ninae mpenzi wangu mmoja ambae nisingependa kuweka jina lake hadharani kwasasa.
February 9, 2011 4:07 PM

Anonymous said...
historia ya Maisha yako(ulizalika wapi, ulisoma wapi,kazi na mtizamo wako wa baadae my be after 5 years)
ANS:
Nilizaliwa hapahapa Dar mwaka 1985 October 4, masomo yangu ya msingi nilipatia MUHIMBILI primary school, then nikachaguliwa kwenda kisutu lakini sikwenda badala yake nikaanzia Form one kwenye shule moja inaitwa KUNDUCHI GIRLS ISLAMIC HIGH SCHOOL, hapo nilisoma mpaka karibia ya Form three nikahamishiwa ST. MARY'S HIGH SCHOOL ndipo hapo nilipomalizia form four, baada ya hapo nikaenda GREEN ACRES mbezi beach for A-level (form 5), sikumalizia hapo nikaenda Uganda shule moja inaitwa HILLSIDE- Bunamwaya na kumalizia CAMBRIDGE TANZANIA ACADEMY na baadae nikajiunga na chuo for BA in MASS COMMUNICATION at St. AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA - MWANZA ila kutokana nna sababu zilizo nje ya uwezo nilipostpone though natarajia kurudi tena chuo hopefully this year insha-ALLAH, plan zangu ni ku-own my company hapo baadae.
February 9, 2011 7:33 PM

Anonymous said...
ningependa kujua histori yako kwa ujumla umezaliwa lini umesoma wp unafanya nn kwa sasa ndoto zako ni nn kitu gani kimekuumiza ktk life yako nn kimekufarahisha sana ktk life yako,mahusiano yako kimapenzi yakoje kwa sasa?
ANS:
Nafkiri mengi nimeyajibu kupitia swali la hapo juu ila kitu kilichowahi kuniumiza sana ni msiba wa baba yangu, na vilivyowahi kunifurahisha ni vingi sana kiasi kwamba siwezi kukumbuka kwakweli.. Niko kwenye mahusiano na mtu ninaempenda sana hiko ndio ninachokijua kuhusu mahusiano yangu kwa sasa.
February 9, 2011 9:05 PM

Anonymous said...
Je una "mwenza"? Nikitaka kukuoa nipeleke posa wapi? Ahmad.
ANS:
Ha haaa... ninae mtu tayari Ahmad!!! siko tayari kuolewa kwasasa kaka, asante kwa offer.
February 9, 2011 9:34 PM

Anonymous said...
Ni mtangazaji gani wa TV kwa hapa TZ unaweza kusema unamkubali sana.... na kwa nini???
ANS:
Swali gumu kidogo kwakweli.. naomba niwe mkweli.. kwasasa NAJIKUBALI mwenyewe, though ni mbaya kidogo kujisifia but ukizungumzia TV PRESENTERS hapa Bongo kwasasa naweza nikasema hakuna anaenishangaza kihiivyoooo!!! wote naona viwango vyao vya kawaida tu sana.. Am just being frank and honest na wala sio kwa ubaya najikubali mwenyewe.
February 9, 2011 9:58 PM

Anonymous said...
una mchumba au BF???? Unaishi kwako au kwa wazazi??????Huo wembamba ni wako au Diet??? unakunywa pombe??? aina gani??? Kwenu mpo wangapi na wewe wangapi??? Unaelimu kiasi gani????? Kabila gani???Chakula ukipendacho ni kipi???
ANS:
Nina BF, kwasasa ninaishi kwangu, huu ndio mwili wangu sijawahi kufanya diet hata siku moja, SITUMII kilevi cha aina yoyote, nakunywa soda, juice, maji na vingine ambavyo si vilevi, kwababa yangu tuko tisa kwasasa mimi nikiwa wa pili kutoka mwisho, ila kwa mama yangu tuko WAWILI tu ambapo ni mimi wa kwanza na mdogo wangu wa mwisho. nilifika mpaka chuo ambapo nilikuwa nachukua bachelor of arts in mass communication but nilipostpone due to some reasons ila natarajia kurudi tena chuo soon hopefully this year insha-ALLAH ili nikamalizie degree yangu. kuhusu kabila yangu MY DAD is MANYEMA kutoka Kigoma, and MAMA yangu ni MNYARWANDA - MTUTSI, mi napenda sana wali aisee hasahasa na samaki huwa sichoki hiko chakula hata kilasiku.
February 9, 2011 11:49 PM

Anonymous said...
Nasikia ulisoma kunduchi girls je ulimalizia pale au ulihama?
ANS:
Ni kweli nilisoma KUNDUCHI GIRLS lakini sikumalizia pale, nilimalizia ST. MARY'S - mbezi Beach.
February 10, 2011 8:31 AM

Catherine said...
Dada Zama, mi naomba kufahamu kuhusu figure yako, ni ya asili au diet? na kama ni diet tuelekeze, you look good Dada.
ANS:
Ndivyo nilivyo hivi mama angu, sina diet wala sijawahi kufanya diet.
February 10, 2011 11:04 AM

Anonymous said...
ok! wengi pia wameuliza but nami pia naomba jua!
1.asili yako wapi yani kabila
2.nn natarajio yako in da life
3.kama mwanamke unategemea siku 1 kuolewa? na kuwa na watoto wangapi?
4.Ni vitu gani huwa unapendelea na vi2 gani hupendi
5.wwe ni wangapi kuzaliwa kwenu kati ya wangapi?
6. ni kwa nni uliingia ktk siasa ili hali ukiwa mdogo hivyo
Dat all By Augustine magessa

ANS:
Mi ni mmanyema kwa kabila, matarajio yangu kuwa mmoja kati ya wanawake wenye mafanikio sana hapa Tanzania with my own company, swala la kuolewa ni MUNGU mwenyewe ndio anapanga, kuhusu watoto natamani MUNGU akinijaalia niwe na watoto wasiopungua watatu lakini yeye ndio mpangaji, napenda sana kukaa na marafiki kubadilishana mawazo, napenda music, nisichopenda kwakweli ni mtu kunifanya mjinga, sipendi Uongo, na zaidi ya yote nachukia dharau sipendi kabisa, kuhusu wangapi nimeshalijibu juu ila kwenye swala la kuingia kwenye siasa sababu kubwa ni kwakuwa ni kitu ninachokipenda.
February 10, 2011 11:11 AM


Anonymous said...
ur eduction background.
ANS:
Nimeshalijibu juu
February 10, 2011 11:42 AM

SALHA MWANDU said...
I KNOW THAT ULIKUA NI M2 WA WA2 SANA ULIPOKUA SHULENI PALE KUNDUCHI GIRLS MANA NDIO TULIKUA PAMOJA, JE BADO NI HVYO HVYO AMA? NATAKA KUJUA ULIPOKUA SKULI NYINGINE ULIKUA NI ZAMA YULEYULE WA KUNDUCHI AMA? UPANDE WA UCHESHI WAKO NA COMEDY ZAKO

ANS:
Ha ha haaa.. umenikumbusha mbali sana aisee, nafkiri ZAMA ni yuleyule.. kwa ambao wamenizoea na wanaonifahamu vizuri (sio kijuujuu) watathibitisha hilo.
February 10, 2011 3:09 PM

RUKIA HARUNA MEZA said...
FANI HIYO YA UTANGAZAJI NDIO IMEKUFAA SANA,MANA SHULE PALE KUNDUCHI ULIELEKEA KUA HVYO SI UNAJIJUA MWENYEWE ULIKUA MTU WA WA2, SWALI LANGU NI HIVI MTANGAZAJI GANI AMBAE UNA MUADMIRE? NA NINGEPENDA KUJUA KAMA UNAPENDA KUIGIZA MANA NNAHAMU NIKUONE PIA KATIKA KUIGIZA UFANYE JAPO FILAMU MOJA

ANS:
Asante nashkuru, kuhusu mtangazaji ninaemuadmire kwakweli ni EPHRAIM KIBONDE, i really admire this guy, ana style yake ya peke yake ambayo inamfanya awe yeye na kila nikimsikiliza ananifanya nicheke.. Kuhusu kuigiza sijalifikiria hilo, nakumbuka nilivyokuwa shule (Kunduchi Girls) nilikuwa nafanya sana hayo mambo but kwasasa sijafikiria kuhusu kufanya hivyo ila tegemea kuniona kwenye filamu moja yoyote though SI LEO WALA KESHO, it will take time kidogo..
February 10, 2011 3:16 PM

Anonymous said...
nilisikia huko nyuma ulishawahi kuchumbiwa je ni kweli na nani?

Sio kweli.
February 10, 2011 4:36 PM

Anonymous said...
ZAMA MIMI NINAOMBI MOJA KWAKO, NAOMBA UTUWEKEE KIPINDI CHAKO CHA "TAKE ONE" KWENYE YOUTUBE, SISI TULIO MBALI NA BONGO TUWEZE KU-ENJOY, MAANA NILIKUWA NAANGALIA SANA WAKATI NIKO BONGO...... KWA SASA NIMEKIMISS SANA KIPINDI CHAKO. NAKIPENDA SANA SANA.

ANGALIA JINSI UTAKAVYOWEZA KUTUSAIDIA, MAANA NAONA MWENZIO DINA ANATUREKODIA 'LEO TENA' NA ANATUWEKEA KWENYE BLOG YAKE, HUKU MAJUU TUNASIKILIZA KWA RAHA ZETU.....

TAKE TIME TO THINK, KAMA UTAHITAJI MSAADA WA KITALAAM,NIKO TAYARI KUKUSAIDIA.
ANS:
Asante sana kwa kufatilia kipindi, tuko pamoja sana.. kuhusu hiyo hoja ntaifanyia kazi aisee, nafkiri ni muhimu sana.. asante kwa kuniamsha, i'll try kufanya hivyo soon though nafkiri ntahitaji msaada wako pia.. unaweza ukaniandikia through zamaradi.takeone@gmail.com ili nipate mail yako na tuweze kusaidiana
Otherwise Asante sana.. tuko pamoja sana!!
February 12, 2011 3:10 AM

Anonymous said...
hi Zama, mi ningependa kujua kwanini uliacha chuo baada ya kusoma mwaka mmoja tu pale SAUT na kuwa miss Mwanza ukaamua kuondoka kabisa, Je? una mpango wa kumalizia elimu yako ya juu coz umesoma mass communication first year peke yake, maamuzi yako ni yapi hapo? classmate SAUT

ANS:
Sikuacha nilipostpone na nitarudi siku si nyingi kumalizia, kuna sababu iliyonifanya nipostpone na si hayo mambo ya umiss ukizingatia ni kitu ambacho sikuendelea nacho baada ya kupigwa stop na baba yangu (U-MISS), so ipo sababu iliyonifanya nipostpone lakini nisingependa kuiweka hadharani (its personal kidogo). ila nitarudi chuo kumalizia miaka yangu iliyobaki.

5 comments:

Anonymous said...

zamaradi mketema mtoto mzuri hua mi nakuzimika ilaa ndo hivo unaee mtuu kwa sasa.so naomba nikulize swali ushawahi kutia nanga rwanda maana umesema kwamba mamaaaako mzazi mrwanda?
kama bado basi karibu rwanda tunakuzimiii kichiziii


fan wako namba mmoja

mdau rwanda makazi remera

Anonymous said...

Dadangu niseme asante kwa ushirikiano wako wa kujibu maswali yetu, keep it up lady.

Anonymous said...

You are alwayz gud mummy. Huwa nakuzimia sn hasa kipindi chako cha take one, japo kwa ss nakimis kwani sina king'amuzi cha startimes. All in all keep it up ili show yako iendelee kuwa nzuri saaaaana. Napenda kuona wasichana wanaojituma ktk fani zao. Mungu akubariki.........

Anonymous said...

Nimefurahi kusikia kuwa hunywi pombe. Rafiki yangu mmoja (RIP) alifariki kwa kansa ya ini akiwa na miaka 23 tu!!!!! Jirani yetu mmoja (RIP)alifariki dunia kwa janga hilo hilo akiwa na miaka 36 tu. Si lazima mtu uwe Mlokole (born again) au Mwislamu ili utambue madhara ya ulevi kiafya, kifedha, kijamii, kiroho na kisaikolojia. Just look around you. Bahati mbaya tunaishi katika jamii ambayo inadhani kuwa kulewa saaana eti ni sifa. Tafiti UK zinaonyesha kuwa ni 18% tu ya wanywaji wa kila siku wanaweza ku-control wingi wa pombe wanaokunywa. Yaani: 82% ya wanywaji wa kila siku hawajui saa ngapi waseme "Stop! Sasa basi." Kwa kina dada, wanaume wengi wana-"take advantage" ya wanawake waliolewa na kuwafanyia kila wanalotaka wakati kina dada hao wakiwa hoi. Utafiti uliofanywa katika miaka ya 1990's Kenya na Kemri unaonyesha zaidi ya 50% ya watu waliolewa walikuwa hawataki kutumia condom wakati wa tendo kwa sababu ilikuwa wanajiona hawajali au hawajielewi. Mimi nimeacha pombe kabisa 2003 na tangu hapo nimepona vidonda vya tumbo vilivyonisumbua kwa miaka mingi. Zama remain strong si lazima ufate mkumbo kwa kila kitu. Marco M.

Anonymous said...

mhmmm sijaona jipya kwakweli maana majibumengi yamekua ayajitoshelezi kabisa na km ulitaka majibu mengine yawe personal basi usingeomba fns wako wakutumie maswali maana mengi yamekua yana tungo tata so ukitaka kuwa superstar km unavyotaka ni lazima kwa sasa uwe makini na unayotaka kufanya ni ushauri tu