Monday, February 28, 2011

MATUKIO KATIKA PICHA.. MECHI YA BONGOFLEVA NA WANAFILAMU!!!

Hii ilikuwa ni nyomi la siku ya mechi ambayo ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kuchangia wahanga wa mabomu ya gongolamboto

Hii ilikuwa ni kamati ya Ufundi kwa upande wa filamu ambao kiukweli kabisa sikuelewa kazi yao ilikuwa nini maana walitundikwa MBILI BILA tena katika style ya Tembo na Sisimizi

Hakuna watu walikuwa na mbwembwe kama watu wa filamu.. kabla ya wachezaji kuingia walitangulizwa hao unaowaona na matunguli yao uwanjani ambapo hiyo ndio kamati ya ufundi iliyoweka kambi yake BAGAMOYO lakini matunda yake hayakuonekana.. kutoka kushoto ni BI MWENDA, MBOTO, DOKII, CHOPA, MZEE CHILO na MZEE MAGALI.

hiki ndio kikosi cha timu ya Bongofleva ambao kwa kuwaangalia tu kiukweli wanaonekana proffessional na wamejipanga, kikubwa hawakuwa na mbwembwe kabisa lakini waliwanyamazisha vibaya watu wa filamu... mh! ila walipania..


WANAFILAMU ndio hao kama unavyowaona na kikosi chao.. Weeeeengiiiiii wenyewe lakini zilikuwa ni mbwembwe za bure tu, mwisho wa siku walirudi vichwa chini.. THOUGH naomba niseme kwamba AKUNA TIMU ILIYOCHANGAMSHA UWANJANI KAMA WATU WA FILAMU.. wao ndio walikuwa na matukio mengi sana ya kufurahisha wakati wanamuziki walikuwa kikazi zaidi..wao ni mpira na wao wao na mpira na walionesha kiwango kwelikweli..

WEMA SEPETU pamoja na JACKY PENTZEL nao walikuwepo ndani ya uwanja
Hapo sura zetu ndogoooo, la kuongea tena hatuna tumeshalishwa magoli yetu tumetulia yaliyokuwa yakiendelea hapo ni maneno ya mkosaji tena katika mazungumzo baada ya habari.. mh! tuliwezwa maana mwenyewe nilikuwa upande wa filamu, kutoka kushoto SAJENT, AUNT EZEKIEL, ZAMARADI MKETEMA, FLORA MVUNGI huyo aliyejishika kichwa pamoja na MONALISA hapo chini...

MSOSI POPOTE ...
DEOGRATIUS SHIJA nae alikuwepo.. kilichonifurahisha ni jinsi WATANZANIA walivyoitikia wito.. kiukweli kabisa ilikuwa ni kitu kizuri sana.. BIG UP kwa watanzania wote, Big up kwa WACHEZAJI WA TIMU ZOTE na pia kwa CLOUDS MEDIA GROUP kwa kuratibu kitu kikubwa kama hiko ambacho matunda yake yameonekana...
kutoka kushoto SAUDA MWILIMA, SAJENT, AUNT EZEKIEL na mimi huko kulia mwenye kofia..
Washabiki..
DIAMOND pamoja na DOGO JANJA wakifurahia ushindi wao...
Timu ya BONGOFLEVA ikiongozwa na H-BABA wakifurahia Goli... walitunyoosha kisawasawa tuliokuwa tunashangilia filamu..
Watu wa filamu tulikabwa sana siku hiyo...hapo mtitu (mwenye nyekundu)akijaribu kufurukuta mbele ya mwana ubongo wa fuleva...
Mstahiki meya wa Ilala JERRY SLAA kushoto pamoja na Mheshimiwa mbunge wa Kinondoni IDDI AZZAN pamoja na RUGE MUTAHABA ambae ndio alikuwa mratibu wa shughuli nzima..


BANANA alikuja na MTOTO WAKE uwanjani.. mwanzoni nilijua huyu mtoto ni wa kike.. and i was so suprised aliponiambia ni MTOTO WA KIUME maana ilibidi nimuangalie mara mbilimbili.. ni kacute sana.. naona product za mzee Zorro sio mchezo
MOHAMMED MWINKONGI (Frank) nae alitia maguu akiwa na mali yake..
hakuna mtu alienichekesha kama MASANJA ambae yeye alichezea timu ya filamu lakini baada ya kufungwa akajifanya kwamba ni MUIMBAJI na sio muigizaji hivyo akajaribu kubadilisha jezi lakini wakamvua na kumrudisha kwenye jezi yake nyekundu..
Kiushabiki zaidi.. NATASHA na mwanae MONALISA, na kule mwanzo mwenye T-shirt ndefu COLETHA..



Hii ilikuwa ni siku nzuri sana aisee, uwanjani kulikuwa na vituko vingi sana especially style ya uingiaji ya wachezaji wa filamu ambapo MASANJA alikuwa akitembea ule mwendo wake wa kizembe wakati JOTI alikuwa akisalimia mashabiki huku akishhtu.. BIG UP kwa WASANII WOTE kwa moyo wao wa kujitolea kwa ajili ya ndugu zetu hawa wa Gongolamboto bila kusahau WATANZANIA waliojitokeza kwa hali na mali pamoja na CLOUDS MEDIA GROUP.. wanastahili pongezi!!!

6 comments:

Mwanaid Rajab said...

wachezaji wa bongo movies tatizo lao mwembe zilikuwa nyiiiiiingi mno alafu hamna lolote mie nilimsubiria jackline wolper but hakucheza coz nae aliniamasisha nikamwone akicheza.
Inaeleekea zamaradi umempenda sana huyo mtoto wa Banana coz umemuongelea mara mbili nzima ktk picha tofauti na kweli ukikaangalia kama kasichana vile??kumbe kavulana lol labda kafanana na mama yake.

Anonymous said...

MHHHHHHHHHHH WEMA SASA NI JIMAMA JAMANI KAPOTEZA UMBO LAKE ZURI!!!!!!!!!!!!!!!! SHUGHULI YAKE KWISHNEY

Anonymous said...

Ni kweli ni mcute na anaonekana kama girl kwa sababu amefanana sana na mama yake Suzie Walele

Anonymous said...

Zama mbona unasusua sana kutuwekea kipindi chako kwenye net???
Ebu fanya mambo bwna, sisi tuliombali na bongo tunatakuona kipindi chako cha "takeone".

Mwenzio Sophia Kessy keshaanza.... Usije achwa nyuma

Anonymous said...

clouds ni the OPORTUNISTS!

sophia mkumbo said...

maneno mengiiiiiiiiiii bongo movie kazi hamna hawana jipya hao